logo

NOW ON AIR

Listen in Live

11 wathibitishwa kufariki katika ajali mbaya iliyotokea katika barabara kuu ya Kisumu-Nairobi

Kamanda wa polisi alibainisha kuwa ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa basi hilo alipokuwa akijaribu kupita.

image
na

Makala29 January 2024 - 07:12

Muhtasari


•Kulingana na kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Nyando Grace Thuo, ajali hiyo ilihusisha basi la Super Metro na lori.

•Thuo alibainisha kuwa huenda idadi hiyo ikaongezeka kwa sababu kulikuwa na watu waliopata majeraha tofauti.

Gari la Super Metro Bus likiondolewa kutoka eneo la ajali eneo la Otho huko Kisumu

Zaidi ya watu 10 wamethibitishwa kufariki akiwemo mtoto kufuatia ajali mbaya ya barabarani iliyotokea katika eneo la Othoo huko Awasi kando ya barabara kuu ya Kisumu Nairobi.

Kulingana na kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Nyando Grace Thuo, ajali hiyo ilihusisha basi la Super Metro na lori.

Basi hilo lilikuwa likielekea Nairobi kutoka Kampala.

Thuo alibainisha kuwa ajali hiyo ilitokea wakati dereva wa basi hilo alipokuwa akijaribu kupita.

"Magari yote mawili yameharibika na tunaweza kusema kwa sasa karibu watu 10 wamekufa, mtoto ambaye ana umri wa miaka 3 hadi 4 alikufa," Thuo alisema.

Alibainisha kuwa huenda idadi hiyo ikaongezeka kwa sababu watu kadhaa ambao walikimbizwa katika hospitali mbalimbali walikuwa na majeraha tofauti.

Mmoja wa maafisa wa Msalaba Mwekundu karibu na eneo hilo ambaye aliarifu Radio Jambo kuhusu kisa hicho alibainisha kuwa ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa nane usiku wa kuamkia Jumatatu.

“Ajali hii ni mbaya, naona maiti kadhaa hapa, basi liligongana na lori lililokuwa limebeba mchele kwa sababu tuliona limetawanyika kila mahali,” alisema.

Mwandishi wa habari ambaye alikusudiwa kuwa ndani ya basi hilo lakini akaikosa alichapisha kwenye kundi moja akimshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yake.

“Namshukuru Mungu sana kwa sababu nilipanga basi kutoka Kisumu, siwezi kusema kilichotokea kwa sababu abiria wengine ambao tulikuwa tumepanga nao walipanda huku mimi nikiwakosa,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved