logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ni vipi Kenya ilipoteza nafasi ya uwenyekiti ya umoja wa Afrika 2017

Siku chache ndizo zinatenganisha umoja wa Afrika kupata kingozi mpya.

image
na Japheth Nyongesa

Makala12 February 2025 - 13:09

Muhtasari


  • Mwaka wa 2017, Kenya ilipoteza dakika za lala salama kwa raia wa Chad Moussa Faki ambaye pia alikuwa waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo.
  • Mwanzoni nchi ya Afrika Mashariki zilikuwa zimekubaliana  na kumuidhinisha Balozi Mohamed lakini ahadi hio haikukumbatiwa wakati wa uchanguzi.

Siku chache ndizo zinatenganisha umoja wa Afrika kupata kingozi mpya.

Kenya ni mojawapo ya mataifa ambayo yamewasilisha mgombeya pamoja na Madagascar na Djibouti.

Hii siyo mara ya kwanza Kenya kuwasilisha mgombea, hali sawia ilikuweko mwaka 2017 wakati rais msitaafu Uhuru Kenyatta alipomteua balozi Amina Mohamed kuwania nafasi hiyo ya kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika.

Zamu hii ikiwa ya mwanasiasa mzoefu katika ulingo wa siasa na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.  kiongozi mwenye historia ya kuwani nafasi ya urais mara tano ila bahati haikusimama upande wake.

Mwaka wa 2017, Kenya ilipoteza dakika za lala salama kwa raia wa Chad Moussa Faki Mahamat ambaye pia alikuwa waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo.

Wakati wa kura ya awamu ya sita nchi za Uganda, Djibouti na Burundi ziliamua kubadili nia na kuchagua kutoipigia Kenya hivyo basi kura hizo tatu zikawa za muhimu kwa nchi ya Chadi. Kenya ikawekwa nje na Chad ikapishana pekee yake awamu ya mwisho na kutwa ushindi.

Mwanzoni nchi za Afrika Mashariki zilikuwa zimekubaliana  na kumuidhinisha Balozi Amina Mohamed lakini ahadi hiyo haikukumbatiwa wakati wa uchanguzi.

Uganda, Burundi na Djibouti wote walimpigia Kenya katika msururu wa kwanza hivyo Mohamed akapa kura 16 dhidi ya Faki 14.

Kura zilizobaki zikawa zimegawanishwa Senegal, Botswana na Equitorial Guinea. katika msururu wa pili Chad ilipata kura 21 huku Kenya wakiongeza moja tu. 

Mahamat aliendeleza ushindi wake katika msururu wa tatu kwa kura 21 dhidi 17 baada ya mataifa jirani ya Kenya kukosa  kuipigia. Hata hivyo kenya ilipata uungwaji mkono tena baada wagombea wa mwisho watatu kujiondoa hivyo mgombea wa kenya akapata 26 dhidi ya Faki ambaye alipata 25.

Kura zilifikia msururu wa sita na Chadi ikavuna na kupata kura 28 dhidi ya Kenya 25. Hivyo Faki akatangazwa mshindi baada kupishana pekee yake katika raundi ya saba na kupata kura 38.

Mataifa ya SADC yalijitenga nsa uchaguzi huo baada kususia mteule wao wa Botswana alipokosa kufanikisha kuendelea mbele kwenye pambano hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved