logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Historia ya siku ya Redio Duniani

Tarehe 13 Februari kila mwaka ni siku ambayo ilitengwa na shirika la umoja wa kimataifa UNESCO kama siku ya redio duniani

image
na Evans Omoto

Makala13 February 2025 - 09:27

Muhtasari


  • Kauli mbiu ya mwaka huu ni  kusherehekea siku ya redio duniani na mabadiliko ya tabianchi,hii ni kuashia kuwa redio ni kiungo muhimu katika kupasha ujumbe unaotokana na utunzi wa mazingira yetu.

Historia ya siku kuu ya Redio Duniani

Tarehe 13 Februari kila mwaka ni siku ambayo ilitengwa na shirika la umoja wa kimataifa UNESCO kama siku teule ya kusherehekea Redio Duniani kutokana na azimio la kongamano la 36 kufanyika mwaka 2011.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni  kusherehekea siku ya redio duniani na mabadiliko ya tabianchi, hii ni kuashiria kuwa redio ni kiungo muhimu katika kupasha ujumbe unaotokana na utunzi wa mazingira yetu.

Hata hivyo tunaposherehekea siku kuu hii ya redio duniani inatufaa kukumbuka vyema kuwa redio ni chombo cha mawasiliano ambacho hutumika kupitisha ujumbe katika hadhira pana na lengwa.

Kwa mfano baadhi ya majukumu ambayo redio ilitumika kuweza kupisha ujumbe ni kuelimisha, redio ilitumika katika miaka ya zamani kuelimisha jamii katika masuala mbalimbali kama vile uongozi,kukashifu vitendo viovu kama ufisadi na kufundisha kuhusu umuhimu wa kuishi kwa Pamoja na kushirikiana.

Vilevile redio ilitumika kama chombo cha kupasha watu na jamii Habari na matukio yaliyokuwa yakijiri kwa mfano kuelezea jamii umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi,umuhimu wa kupokea chanjo na tiba iliyotolewa na serikali na vilevile kuonya kuhusu masuala ambayo yangeleta madhara kwa jamii au vita.

Redio kama chombo kilichotumika kuelimisha,kupasha  ujumbe vilevile   kutumika kama chombo cha burudani kwa kucheza miziki kwa mshabiki miziki ambayo ilinuia kukuza tamaduni za jamii na zile za uzalendo ambazo zililenga kuwashirikisha na kuwaleta wananchi kwa Pamoja.

Redio kwa miaka mingi ilikuwa na imekuwa mhimili imara kwa jamii kwa kueleza na kuwazindua wananchi kwa kuwafundisha mambo mengi wasioyafahamu  katika jamii.

Karne ya sasa kuna aina nyingi za redio  ambazo zinaendeleza jukumu la kuelimisha na kuwapa wananchi nafasi ya kujieleza ipasavyo kwa kutumia uhuru wa kujieleza katika Redio.

Katika taifa la Kenya Redio ilianzishwa mwaka wa 1927 kama redio ya Afrika mashariki (EABC) ambapo redio hiyo ilikuwa ikitangaza Habari za BBC kwa wazungu.

Mnamo mwaka wa 1953 baada ya vita vya pili vya dunia Redio ya ABS ilianzishwa ikitangaza kwa lugha ya Kiswahili na Luo na baadhi ya lugha za mama.

Hatimaye mwaka wa 1959 kituo cha KBS(Kenya Broadicasting services) kilizinduliwa na ulipofika mwaka wa 1964 KBS ilibadilishwa jina na kuitwa VOK ambapo ulipofika mwaka wa 1989 bunge la taifa la Kenya lilirudisha jina KBC.

Katika nchi ya Kenya kwa sasa kuna jumla ya Redio 303 kulingana na mujibu wa mamlaka ya mawasiliano nchini Kenya(CAK) ambapo kwa Redio hizo kuna zile za binafsi, redio zinazomilikiwa na mashirika ya serikali na zile za viwango vya Jamii.Baadhi ya redio nchini ni Radio Jambo,Radio Citizen,KBC Radio Taifa,Radio Maisha,Radio 47 na Milele fm.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved