logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Valentine's Day' ni kilele cha upendo duniani

Siku hiyo ilibadilishwa na kuitwa mtakatifu Valentino baada ya kufungwa jela kwa mtakatifu Valentino kutokana na kupenda mtoto wa kike.

image
na Evans Omoto

Makala13 February 2025 - 09:54

Muhtasari


  • Inasemekana kuwa katika enzi ya istimari katika karne ya tano paliondokea mtakatifu mmoja kwa jina papa Gelasius kule Roma aliyekuwa katika hafla ya sherehe.
  • Baada ya kuonyesha upendo kwa huyo mwanadada siku hiyo licha ya sheria iliyokua wakati huo kupinga mtumishi wa Mungu siku hiyo ilibadilishwa na kuitwa Valentine.

Siku kuu ya Valentino duniani 14 Februari,2025

Naam katika kulizamia  swala hili na kufahamu kwa ufupi ni nini chanzo na maana ya valentino naomba tusafiri na wewe katika kujua chimbuko lake.

Inasemekana kuwa katika enzi ya istimari katika karne ya tano paliondokea mtakatifu mmoja kwa jina papa Gelasius kule Roma aliyekuwa katika hafla ya sherehe.

Inasemekana kuwa akiwa katika hafla hiyo alimuona msichana mmoja kipofu utu ukamvaa akamkumbatia na kumwona kama mtu wa muhimu sana katika sherehe hiyo iliyoitwa Lupakalia.

Baada ya kuonyesha upendo kwa huyo mwanadada siku hiyo licha ya sheria iliyokua wakati huo kupinga mtumishi wa Mungu kuwa na mahusiano au nia ya kupenda.

 Siku hiyo  ilibadilishwa na kuitwa mtakatifu Valentino baada ya kufungwa jela kwa mtakatifu Valentino kutokana na kitendo cha sheria kali za Kirumi ambazo zilikuwa kinyume na masuala ya mahusiano katika karne ya tatu.

Hatimaye watu walibadilisha fikra na kuiona siku hiyo ya 14 ambapo mfia dini mkuu wa kikristo alifanya kitendo cha kuoa, watu wakaitambua siku hii kama siku ya upendo duniani.

Mataifa mengi duniani yakaiga mtindo huo yakaanza  kusherehekea siku hio kwa namna mbalimbali kwa kuweza kuwapa kumbukizi na fikra za kuonyesha upendo kwa wapenzi,marafiki,jamaa na wazazi.

Baadhi ya mataifa ambayo husherehekea siku hii duniani ni Marekani,Uingereza,Kanada, Australia,Ajentina,Ufaransa,Mekisko na Korea Kusini yakiwemo mataifa ya  Afrika.

Hata hivyo watu wanapojiandaa kusherehekea siku hii ya Valentino mnamo Februari 14,2025 wengi watatarajia kupokea zawadi mbalimbali yakiwemo maua na mapambo mengi sana kuashiria upendo.

Kwa hivyo kuna watu wengi ambao huwa wanasawiri siku hii kama siku ya mapenzi kwa wale ambao wanapendana pekee  ila badala yake siku hii inasitahiki kuleta mabadiliko katika maisha ya watu wengine ili siku hii iwe ya kukumbukwa daima.

Siku ya Valentino licha ya kuwa ni siku ambayo imesheheni upendo kuna watu ambao wanaitumia siku hii kuweza kuonyesha upendo wa dhati kwa wazazi,wapenzi wao, Watoto mayatima,wazee na kina Mama wajane ili wahisi umuhimu wa siku hio adhimu.

Kuna watu mbalimbali ambao watatumia siku ya Valentino kuweza kuzuru magereza mbalimbali ili kuonyesha upendo kwa wafungwa na wagonjwa katika hospitali mbalimbali ili kuwaombea dua ya kupona kwa Mungu, wacha iwe siku ya heri na fanaka kwa sisi sote.

Wengi wameratibu kuweza kuzuru shule mbalimbali kwa ajili ya kuwapokeza visodo Watoto wa kike ambao wanatoka katika Jamii zizizojiwza ili nao waweze kuhisi wanapendwa na kuthamini siku hii ya Valentino,kutoka kwangu mimi pia nakutakia Valentine njema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved