logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mamia wakimbia makazi yao Laikipia kufuatia ghasia

Kamishna wa eneo la Bonde la Ufa,George Natembeya amedai wavamizi hao wana bunduki aina ya M16 , ambazo haziuzwi nchini humo.

image
na Radio Jambo

Habari08 September 2021 - 09:41

Muhtasari


•Mamlaka imeonyesha wasiwasi juu ya watu wenye silaha ambao walikuwa wanapambana na polisi.

•Kamishna wa eneo la Bonde la Ufa,George Natembeya amedai wavamizi hao wana bunduki aina ya M16 , ambazo haziuzwi nchini humo.

Mamia ya watu wamekimbia makazi yao wakati ghasia zilipotokea katika hifadhi ya Laikipia iliyopo bonde la Ufa nchini Kenya.

Mamlaka imeonyesha wasiwasi juu ya watu wenye silaha ambao walikuwa wanapambana na polisi.

Zaidi ya watu 12 wameuawa, wakiwemo sita waliouawa wiki jana

Milio ya risasi ilisikika majira ya mchana, moshi ukionekana huku polisi wakisema ghala la shule moja liliteketea na wanafanya uchunguzi kuhusu tukio hilo .Kupitia taarifa polisi wamesema wanafunzi hawakuwa katika shule hiyo ya Merigwiti iliyodaiwa kuchomwa katika ripoti za vyombo vya habari hapo awali nchini humo .

Wakazi wamekuwa wanakimbia makazi yao ambayo wamekaa kwa miongo kadhaa.

Washambuliaji katika hifadhi binafsi ya Laikipia pia wanalisha mifugo yao kwa jeuri kwenye mashamba ya mahindi ya wakulima wasio na ulinzi.

Kamishna wa eneo la Bonde la Ufa,George Natembeya amedai wavamizi hao wana bunduki aina ya M16 , ambazo haziuzwi nchini humo.

Polisi wa Kenya huwa wanatumia bunduki za G3 na AK47, ambapo mara nyingine watu wasiokuwa na vibali hutumia kufanya ujambazi.Wamesema wanaendelea na oparesheni ya kurejesha utulivu


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved