logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vurugu zazuka katika mkutano wa Azimio Mombasa baada ya Sonko kuwasili

Magari ya Sonko kisha yakageuka huku umati ukitawanyika.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 May 2022 - 14:06

Muhtasari


  • Vurugu vyazuka katika mkutano wa Azimio Mombasa baada ya Sonko kuwasili

Vurugu vilikumba kwa muda mkutano wa Azimio wa Raila Odinga huko Mkomani mjini Mombasa baada ya aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko kuwasili

Magari ya Sonko yaliwasili katika ukumbi wa Mkomani wa mkutano huo mwendo wa saa 3.30 jioni.

Magari yake mawili yalijaribu kuelekea upande wa pili wa ukumbi uliokuwa na watu wengi huku wawaniaji tofauti wakijitambulisha.

Gavana wa Mombasa Hassan Joho alilazimika kukatiza utambulisho huo mara kadhaa alipokuwa akiwahutubia madereva kutosogeza magari hayo.

"Juma, usisogeze magari, yaweke hapo yalipo, unaenda wapi?" Joho aliendelea kuuliza.

Joho alijaribu kutuliza umati lakini kelele ziliendelea kupanda, huku gari la Sonko likiendelea kupita katikati ya umati.

Mambo yote yalizuka baada ya mawe kuonekana yakiruka kati ya umati, na kuwalazimu polisi kuingilia kati huku wakifyatua risasi hewani kujaribu kutawanya sehemu ya umati iliyokuwa ikizidi kuwa mbaya.

Magari ya Sonko kisha yakageuka huku umati ukitawanyika.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved