logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Elachi:Kwa nini Uhuru, Ruto lazima warudi nyumbani

"DP na Rais wangu lazima waende nyumbani na sisemi kwa sababu niko Azimio,

image
na

Yanayojiri23 June 2022 - 09:56

Muhtasari


  • Elachi alisisitiza kuwa viongozi wazuri ambao wana nia ya dhati ya Kenya watasaidia kurejesha uthabiti wake wa kisiasa na kiuchumi
Katibu mkuu mwandamizi katika kitengo cha jinsia ya umma, Beatrice Elachi.

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Kaunti ya Nairobi Beatrice Elachi amesema kuwa Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wanahitaji kurejeshwa nyumbani.

Akiongea na NTV siku ya Alhamisi, Elachi alieleza kuwa ili Kenya ipate uvumilivu wa kisiasa ilikuwa imefika wakati maafisa hao wawili wakuu waondoke afisini na kutafuta watu wapya.

Aliongeza kile ambacho Kenya inahitaji ni kuangazia upya na kujenga upya kama ilivyokuwa mwaka wa 2002.

"DP na Rais wangu lazima waende nyumbani na sisemi kwa sababu niko Azimio, nasema hivyo ili tuielekeze tena nchi hii, tuirudishe 2002 na kuanza nayo safari," alisema.

Elachi ambaye anawania kiti cha ubunge cha Dagoretti Kaskazini aliongeza kuwa ni jukumu la kibinafsi kuhakikisha kuwa viongozi makini wanachaguliwa katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9, mwaka huu.

Elachi alisisitiza kuwa viongozi wazuri ambao wana nia ya dhati ya Kenya watasaidia kurejesha uthabiti wake wa kisiasa na kiuchumi.

Aliteta kuwa kutokana na rasilimali chache zinazopatikana serikali za kaunti na kitaifa lazima zifanye juhudi ili afisi zifanye kazi inavyopaswa.

"Utekelezaji ipasavyo wa sheria utawaongoza wale waliochaguliwa ofisini kwa manufaa ya taifa," aliongeza.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved