logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hamna tofauti yenu na magaidi,Kindiki awaambia wezi wa mifugo huku akiwaonya

Kindiki alisema tayari wameanza kazi ya kuwatafuta na watawapata muda si mrefu.

image
na

Makala25 November 2022 - 08:25

Muhtasari


  • Waziri huyo alisema kuwa majambazi hao wamewatia watu hofu kwa muda mrefu na hawakuadhibiwa lakini ni wakati wao wa kulipa

Waziri wa Usalama wa Ndani amesema wameweka hatua kali kukabiliana na wezi wa mifugo huko Isiolo.

Akiongea na wakazi wa Isiolo siku ya Alhamisi, Kindiki alisema hataruhusu wezi hao kuwatisha watu na watasaka eneo hilo kwa makini hadi wawapate

"Ninataka kukuhakikishia kwamba tumepata habari kuhusu waliko na tunawatafuta," alisema.

"Tutawaadhibu na kuwachukulia hatua kwa sababu hakuna fisadi na mwizi, na hakuna jambazi ambaye ana nguvu za kutosha kuishinda serikali."

Kindiki alisema tayari wameanza kazi ya kuwatafuta na watawapata muda si mrefu.

“Tutawatafuta hao wezi, lazima tuhakikishe ulinzi unarudi na kwa majambazi siku zenu zinahesabika,” alisema.

Waziri huyo alisema kuwa majambazi hao wamewatia watu hofu kwa muda mrefu na hawakuadhibiwa lakini ni wakati wao wa kulipa.

“Wanaoiba mifugo na kuua watu hakuna tofauti kati yenu na magaidi,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved