logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ujumbe wa Ruto kwa Wakenya huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya wanawake

Ruto alisema anategemea uungwaji mkono wa wanawake wa Kenya ili kufikia usawa wa kijinsia.

image
na Radio Jambo

Makala08 March 2023 - 09:35

Muhtasari


  • Rais Ruto alikariri kujitolea kwa utawala wake kutimiza ahadi ya kujumuishwa kwa sababu ni muhimu kwa maendeleo ya nchi

Huku uimwengu ukiadhimisha siku ya wwanawake duniani, Rais William Ruto alikuwa na ujumbe kwa wanawake na Wakenya kwa jumla.

Katika ujumbe wake, Rais alisema anajivunia hatua iliyofikiwa na utawala wake katika kuhakikisha ushirikishwaji wa wanawake katika uongozi.

Rais Ruto alikariri kujitolea kwa utawala wake kutimiza ahadi ya kujumuishwa kwa sababu ni muhimu kwa maendeleo ya nchi.

"Hii ndiyo sababu nimeshiriki uongozi wa bunge kwa nia ya kuchukua hatua za pamoja za uzalendo wa pande mbili kutafuta njia ya kikatiba ya kukuza usawa na ushirikishwaji katika uwakilishi wa kisiasa," alisema.

Alisema pia amejipanga kuondoa vikwazo vyote vinavyokwamisha maendeleo ya kufikia usawa wa kijinsia.

Ruto alisema anategemea uungwaji mkono wa wanawake wa Kenya ili kufikia usawa wa kijinsia.

"Pia tunajitolea kuondoa vizuizi vya kimfumo na kusalia mkondo kuelekea usawa kwa wote nchini Kenya tukiwa na imani kwamba ushiriki kamili wa wanawake unaweza kutusaidia kutambua nusu inayokosekana ya bidhaa ya kitaifa ya nchi yetu. Heri ya Siku ya Wanawake."

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved