logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Musalia Mudavadi amtembelea aliyekuwa naibu Rais Moody Awori

Mudavadi alimsifu kwa kuwa imara na shupavu.

image
na Radio Jambo

Makala13 March 2023 - 09:44

Muhtasari


  • Kulingana na Mudavadi, ilikuwa ishara nzuri kumpata kwa sababu walibadilishana masuala kadhaa ambayo viongozi wanapaswa kuzingatia katika nchi yetu.

Mkuu wa Mawaziri  Musalia Mudavadi leo amemtembelea aliyekuwa Makamu wa Rais Moody Awori katika makazi yake Nairobi.

Kulingana na Mudavadi, ilikuwa ishara nzuri kumpata kwa sababu walibadilishana masuala kadhaa ambayo viongozi wanapaswa kuzingatia katika nchi yetu.

Mudavadi alimsifu kwa kuwa imara na shupavu.

"Ilikuwa ni ishara ya kupendeza kukutana naye tulipojadiliana kuhusu masuala kadhaa ambayo tunapaswa kuzingatia kama nchi; miongoni mwao hitaji la kukuza umoja na utangamano endelevu miongoni mwa Wakenya na kufanyia kazi utekelezaji wa manifesto ya Kenya Kwanza.

Sisi pia ilichukua muda kutafakari siku tulizohudumu pamoja serikalini. Katika umri wake, Mzee anabaki imara na shupavu." Aliandika Mudavadi.

Haya yanajiri siku chache baada ya makamu huyo wa zamani kukutana na Katibu mkuu wa muungano wa wafanyikazi nchini Francis Atwoli, mwanasheria mkuu mstaafu na ambaye pia alikuwa seneta wa Busia Amos pamoja na aliyekuwa mbunge wa Westlands Fred Gumo

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved