logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto afufua mradi wa ujenzi wa mabwawa ya Kimwarer na Arror

"Mchakato wa kutatua masuala mahakamani tayari umeanza kwa dhati," Ruto alibainisha.

image
na Radio Jambo

Makala14 March 2023 - 10:05

Muhtasari


  • Aliongeza kuwa hatua zitachukuliwa kujadili upya urekebishaji wa fedha zilizofanywa wakati wa uongozi wa Rais mstaafu Uhuru Kenyatta
Rais William Ruto akitoa marufuku kwa wafugaji kutumia bunduki.

Rais William Ruto mnamo Jumanne, Machi 14, alitangaza kuanzishwa tena kwa mazungumzo kuhusu ujenzi wa mabwawa ya Kimwarer, Arror na Itare katika eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa.

Akizungumza wakati wa kikao na wanahabari baada ya mkutano na Rais Sergio Mattarella wa Italia katika Ikulu ya Nairobi, Mkuu wa Nchi alibainisha kuwa serikali itashirikiana na serikali ya Italia kuondoa vikwazo vinavyozuia maendeleo ya miradi hiyo.

Rais Ruto alithibitisha kuwa serikali zote mbili zilikubali kuwezesha uondoaji wa kesi zinazopinga uhalali wa mchakato wa ununuzi unaofuatwa katika hatua za awali za miradi hiyo.

"Mchakato wa kutatua masuala mahakamani tayari umeanza kwa dhati," Ruto alibainisha.

“Tumekubaliana kuanzisha tena ushirikiano katika ujenzi wa mabwawa ya Arror, Kimwarer na Itare na miradi mingine ya maji na usafi wa mazingira ambayo ni muhimu kwa ajenda yetu ya usalama wa chakula, utoaji wa maji na hatua za hali ya hewa,” alisema Rais.

Aliongeza kuwa hatua zitachukuliwa kujadili upya urekebishaji wa fedha zilizofanywa wakati wa uongozi wa Rais mstaafu Uhuru Kenyatta.

Kulingana na Ruto, serikali ilikuwa na nia ya kuhakikisha kuwa mradi wa Arror na Kimwarer utaanza tena baada ya mwezi mmoja, na kuitaja kama "dharura na kipaumbele" kwa mipango ya serikali ya kupunguza shida ya uhaba wa maji katika maeneo ya Bonde la Ufa. .

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved