logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KANU: Hatuwatambui wanachama waliohamia UDA

Aliyekuwa Katibu mkuu wa KANU ,Nick Salat aljiung na cham cha UDA pamoja na wanachama wengine.

image
na

Makala16 March 2023 - 11:28

Muhtasari


• Goerge Wainaina alisema kuwa KANU haitawachukulia kirahisi watu wanaojaribu kuchafua jina la chama.

Katibu mkuu wa Kanu Nick Salat.

Viongozi wa chama cha KANU sasa wamesema kwamba hawawatambui wanachama waliogura chama hicho na kuingia kwa chama cha UDA.

Viongozi hao walisema hilo baada ya baadhi ya viongozi wa KANU akiwemo Nick Salat kujiunga na chama cha UDA wakiwa wamevalia nguo za KANU kuashiria kuwa chama hicho kimejiunga na chama cha UDA.

Katibu mkuu wa KANU, George Wainanina ,alisema kuwa wanachama wa KANU waliobaki hawatagura kujiunga na chama chochote kama alivyofanya Nick Salat na wanachama wwengine.

Katibu mkuu huyo alisema kuwa wanaodai kuwa walikuwa wanachama wa KANU waliandikwa hivyo basi hawafai kutambulishwa kama wanachama wa chama hicho.

"Kinachotushtua ni matumizi  mabaya ya bidhaa za chama chenye thamani kubwa kuomba makombo ya mkate kutoka kwa serikali iliyojaa hadi ukingo  na wahusika waliokodishwa ," ilisoma sehemu ya taarifa hiyo.

Katibu mkuu Wainaina ailizidi kumnyooshea kidole Salat kwa kuendesha sarakasi, aikithibitisha kuwa  chama hicho hakitawachukulia kirahisi watu wanaojaribu kuchafua jina la chama.

Aliongeza kuwa chama hakijachanganyikiwa na hatua hiyo inayodaiwa . "Kile ambacho hatutasema uwongo ni watu binafsi kuhamaki kutoka mkutano mmoja hadi mwingine, kuwahadaa Wakenya chini ya uficho wa chama chetu tunachopenda," akabainisha.

"Tunataka kuwaambia kwamba KANU, iliyojengwa kwa msingi imara sana, haijaguswa na uasi wao unaodaiwa." Alisema kuwa KANU itasalia kujitolea kusalia imara na umoja katika kukuza demokrasia, umoja wa kitaifa na haki ya kijamii.

Siku ya Jumatano, Salat alidai kuwa ameongoza timu kutoka KANU hadi UDA, na kwamba wengine pia wana nia ya kuhama.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved