logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sakaja atia mkataba wa maendeleo na Afrika Kusini

Kusini na Mashariki zimeunga kuendeleza utendakazi

image
na

Habari23 May 2023 - 12:18

Muhtasari


•Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja ametia sahihi  mkataba wa maendeleo na Hill-Lewis ambaye ni meya wa Cape Town  Afrika Kusini Jumanne 23.

•Sakaja, ambaye kauli yake wakati wa kampeni ilikuwa  “wacha tufaifanye  Nairobi ifanye kazi”,amekuwa akiendeleza kauli hiyo hasa kwa  baraza la kata hiyo kwa kuwapa magari mapya ndipo kufanikisha maendeleo.

Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja ametia sahihi  mkataba wa maendeleo na Hill-Lewis  meya wa mji wa Cape Town  Afrika Kusini.

Sakaja, ambaye kauli yake wakati wa kampeni ilikuwa  “wacha tufaifanye  Nairobi ifanye kazi”,amekuwa akiendeleza kauli hiyo hasa kwa  baraza la Kaunti hiyo kwa kuwapa magari mapya ndipo kufanikisha maendeleo.

 Katika mitandao yake ya kijamii alisema kuwa ,“Nina furaha kwa kuusaini mji dada wa Cape Town  kwa makubaliano na utawala wa meya  Hill-Lewis hivi leo. Nairobi na Cape Town ni majimbo makubwa katika bara letu.”

Sakaja  aliendelea na kusema kuwa, kusini na mashiriki mwa Afrika zimeungana pamoja ndipo kuendeleza utendakazi.Haya yanajiri huku baadhi ya vikwazo vilivyoyakumba mataifa haya mawili kuondolewa, ambapo gavana huyo alitaja kama nafasi  nzuri kwa watu katika mataifa yote mawili.

“Ushirikiano huu tumeafikiana kuondolewa kwa baadhi ya visa kati ya nchi hizi mbili na ambayo ni nafasi kubwa kwa watu.” Sakaja alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved