logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa wawili wakamatwa kwa madai ya kuiba Sh8 milioni

Kesi hiyo iliripotiwa mwishoni mwa mwezi uliopita na mke wa mfanyabiashara huyo.

image
na Radio Jambo

Habari23 May 2023 - 12:41

Muhtasari


  • Ksh. Milioni 2.5 zimepatikana kutoka kwa washukiwa hao wawili huku msako mkali wa kumsaka mshukiwa wa tatu David Mushendu ambaye bado hajakamatwa.

Washukiwa wawili wamekamatwa kwa madai ya kuiba Ksh.8 milioni kutoka kwa mfanyabiashara wa Kiambu.

Kulingana na taarifa ya Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) pesa hizo ziliibwa kutoka kwa sefu iliyokuwa imefichwa katika kituo cha pampu kilichotelekezwa eneo la Kinangop, Kaunti ya Nyandarau.

Kesi hiyo iliripotiwa mwishoni mwa mwezi uliopita na mke wa mfanyabiashara huyo.

"Katika tukio lililoripotiwa mwishoni mwa mwezi uliopita na mke wa mfanyabiashara huyo, pesa hizo ziliibiwa kwenye sefu," ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.

DCI ilibaini kuwa washukiwa hao wawili, Moses Cherish na Eliud Wangai, waliingia kwenye jengo hilo kupitia paa na kuiba pesa hizo.

"Washukiwa hao wanaaminika kuwa waliingia ndani ya jengo hilo kupitia paa kabla ya kujisaidia na pesa hizo baada ya kuvunja sefu," DCI iliripoti.

Ksh. Milioni 2.5 zimepatikana kutoka kwa washukiwa hao wawili huku msako mkali wa kumsaka mshukiwa wa tatu David Mushendu ambaye bado hajakamatwa.

Watuhumiwa hao wawili wanakabiliwa na mashtaka ya wizi kinyume na kifungu cha 281 cha sheria ya kanuni ya adhabu.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved