Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Multimedia ajitia kitanzi katika bafu ya bweni

Marehemu alikuwa akisoma Hisabati na Sayansi ya Kompyuta chini ya kitivo cha Sayansi na Teknolojia.

Muhtasari

• Vyanzo vya habari kutoka shuleni vilisema kuwa marehemu alipatwa na mmoja wa wahudumu wa nyumba hiyo Jumapili asubuhi.

• "Mwili wake ulipatikana ukining'inia kwenye boriti kwenye chumba cha kuogea cha hosteli Jumapili asubuhi," 

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Multimedia ajitia kitanzi
Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Multimedia ajitia kitanzi
Image: HISANI

Mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada  kutoka Chuo Kikuu cha Multimedia  alipatikana amefariki katika chumba cha kuogea cha hosteli.

Mkuu wa polisi wa Nairobi Adamson Bungei alisema wanafahamu mkasa huo na uchunguzi unaendelea kuhusiana na hilo.

"Mwili wake ulipatikana ukining'inia kwenye boriti kwenye chumba cha kuogea cha hosteli Jumapili asubuhi," alisema

Vyanzo vya habari kutoka shuleni vilisema kuwa marehemu alipatwa na mmoja wa wahudumu wa nyumba hiyo Jumapili asubuhi.

"Alikuwa mcheshi. Hakuna jinsi mtu angeshuku kuwa alikuwa na mawazo kama hayo," chanzo kiliambia shirika la The Star.

Marehemu alionekana mara ya mwisho kwenye mtandao wa WhatsApp mwendo wa saa 1:35 asubuhi siku ya Jumapili.

Mmoja wa wanafunzi wenzake, hata hivyo, alisema kuwa alikuwa akitizama filamu hadi usiku wa manane.

Walio karibu na marehemu walisema alikuwana mahangaiko ya kifedha.

Marehemu pia anasemekana kuwa na matatizo na masomo yake hata alijaribu kurudia mwaka wake wa tatu wa masomo ili kuongeza alama zake.

"Mwanzoni mwa muhula hakutaka kuhitimu na kufaulu. Hivyo alipendekeza arudie mwaka wa tatu ili angalau aongeze alama zake. Lakini kwa jinsi shule inavyoendeshwa haikuwezekana," mshirika wake wa karibu alisema.

Marehemu alikuwa akisoma Hisabati na Sayansi ya Kompyuta chini ya kitivo cha Sayansi na Teknolojia.

Shule hiyo imepanga kufanya tukio la uhamasishaji wa afya ya akili siku ya Jumatano ili kuwachukua wanafunzi katika kudhibiti unyogovu.

"Kesho shuleni kutakuwa na tukio la afya ya akili. Kwa kawaida tunakuwa nalo kila muhula, lakini muhula huu wameona umuhimu wa kufanya hivyo mapema kwa sababu ya tukio hili," chanzo kilisema.

Naibu chansela Prof Paul Mbatia alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema:

"Tumeweza kumfikia baba lakini bado hatujafika kwa mama kwa hivyo hatuwezi kutaja majina," Mbatia aliambia Citizen digital.

Marehemu alipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha City ambako uchunguzi wa maiti utafanywa.