Hakuna msamaha au fidia? Savara wa Sauti Sol anahoji baada ya ziara ya Mfalme Charles

Huku akikiri kuwa mfalme alizungumzia dhuluma za zamani zilizofanywa na Waingereza kwa Wakenya, hakukosa kutambua kwamba hakuomba msamaha.

Muhtasari

• Mfalme Charles III ambaye alikuwa nchini kwa ziara ya kiserikali alishinikizwa kuomba radhi kwa ukatili uliofanywa nchini humo na Waingereza wakati wa utawala wa kikoloni.

Charles na Savara
Charles na Savara
Image: X

Savara Mudigi wa Sauti Sol ametoa hisia tofauti baada ya ziara ya hivi majuzi ya Mfalme Charles nchini Kenya.

Mwanamuziki huyo katika chapisho lake Jumamosi kupitia akaunti yake ya X alisema alipata nafasi ya kukutana na Mfalme na wakazungumza kuhusu mapenzi yao kwa muziki.

Huku akikiri kuwa mfalme alizungumzia dhuluma za zamani zilizofanywa na Waingereza kwa Wakenya, hakukosa kutambua kwamba hakuomba msamaha.

Hata hivyo aliitaja ziara ya Mfalme huyo kuwa ya kuvutia licha ya kutoomba msamaha na kutozungumzia fidia.

"Nilikutana na Mfalme Charles. Tulizungumza kuhusu kupiga ala. Ngoma zangu na bendi ya cello. Ziara ya Mfalme nchini Kenya imekuwa ya kuvutia, alizungumza juu ya ukatili uliofanywa na Waingereza kwa Wakenya wakati wa ukoloni na akataja kuwa hauna udhuru, haikuwa kuomba msamaha na hakuna mazungumzo ya fidia," Savara alisema.

"Bado ninapingana kuhusu umuhimu wa hili lakini bado ni maendeleo kidogo. Kenya sasa ina miaka 60. Naomba tuishi kuwa elfu na zaidi," alisema.

Mfalme Charles III ambaye alikuwa nchini kwa ziara ya kiserikali alishinikizwa kuomba radhi kwa ukatili uliofanywa nchini humo na Waingereza wakati wa utawala wa kikoloni.

Maelfu wanasemekana kupoteza maisha wakati wa Dharura ya Mau-Mau katika miaka ya 1950 hata wengine waliachwa bila makao baada ya kufurushwa kutoka kwa ardhi hiyo.

Wapiganaji na wafuasi kadhaa wa Mau Mau pia walizuiliwa kwa wingi.

Wiki iliyopita, Kamishna Mkuu wa Uingereza Neil Wigan alieleza ni kwa nini Uingereza haitaomba msamaha kwa Kenya kutokana na ukatili uliofanywa wakati wa ukoloni.

Wigan alisema ni vigumu sana kuomba msamaha, na ndiyo sababu bado hawajaomba msamaha.

Kamishna Mkuu alisema kuomba msamaha kutaleta msingi mgumu wa kisheria kwa serikali ya Uingereza.

Alibainisha kuwa pamoja na hayo, pande zote zilichagua suluhu nje ya mahakama kuhusu suala hilo, jambo ambalo lilionyesha uaminifu wa serikali ya Uingereza.

"Msamaha unaanza kukupeleka katika eneo gumu la kisheria hivyo kusema na makubaliano tuliyoyafanya yalikuwa ni masuluhisho ya nje ya mahakama kwa hiyo yalionyesha ukweli na uwazi wetu kutambua kuwa unyanyasaji umefanyika na hiyo ndiyo njia tuliyoichagua na kuwataka wafanye hivyo. ilikubaliwa na Chama cha Mau Mau Veterans Association," Wigan alisema kwenye Spice FM.