logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Haiti lazima: Bunge lapitisha pendekezo la kupelekwa kwa polisi 1000 nchini Haiti

Ruto alisema Kenya kupeleka polisi Haiti ni moja ya kuafikia takwa la UN kuhusu usalama wa kikanda.

image
na Radio Jambo

Habari16 November 2023 - 09:23

Muhtasari


• Katika kura ya asubuhi siku ya Alhamisi, wabunge walipitisha ripoti ya kamati za pamoja ambayo ilikuwa imependekeza kwamba Bunge liidhinishe kutumwa kwa polisi Haiti.

Makurutu wa polisi

Wabunge katika bunge la kitaifa asubuhi ya Alhamisi walipitisha hoja inayolenga kupelekwa kwa maafisa 1000 nchini Haiti kwa ajili ya kuongoza oparesheni ya kurudisha Amani na usalama mitaani.

Katika kura ya asubuhi siku ya Alhamisi, wabunge walipitisha ripoti ya kamati za pamoja ambayo ilikuwa imependekeza kwamba Bunge liidhinishe kutumwa kwa polisi Haiti.

“Kamati baada ya kukagua wajibu wa Kenya kwa Umoja wa Mataifa, mfumo wake wa kisheria uliopo, mawasilisho kupitia ushirikishwaji wa umma na mawasilisho ya washikadau inapendekeza kwamba Bunge liidhinishe mapendekezo ya kutumwa kwa Huduma ya Kitaifa ya Polisi kwa Misheni ya Kimataifa ya Usaidizi wa Usalama (MSS) kwa Haiti chini ya masharti. ya Katiba,” timu ya pamoja ilipendekeza.

Hii ni baada ya serikali ya Kenya kusema kwamba ilikuwa radhi kuchangia katika usalama wa nchini hiyo ya Carrebean ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikisumbuliwa na magenge hatari.

Kuitishwa kwa pendekezo hilo sasa kunatoa ruhusa kwa maafisa wa polisi kutolewa katika kila kituo cha polisi kote nchini ili kujenga timu ya angalau polisi 1000 katika misheni hiyo.

Uamuzi wa serikali kutuma wanajeshi hao umeonekana kuwa wa kutatanisha na tayari wakili alikuwa ameenda mahakamani akitaka kusimamisha kabisa kutumwa kwa wanajeshi hao.

Mapema mwezi jana, Radiojambo.co.ke ilielewa kwamba idara ya polisi NPS ilikuwa imetoa mwongozo wa jinsi maafisa hao 1000 watakavyopatikana kwa ajili ya misheni hiyo.

Mwongozo huo ulitaka kila afisa mkuu katika kila kituo cha polisi kote nchini kupendekeza angalau maafisa 2 kutoka kila kituo kote nchini ili kutengeneza kikosi cha maafisa 1,000 kwenda Haiti.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved