Vyeti vya 2022/23 viko tayari - KNEC yasema

Knec ilisema vyeti hivyo vimetumwa kwa shule ambako watahiniwa walifanya mitihani yao

Muhtasari

•KNEC ilisema vyeti vya KCSE 2022, 2022 na 2023 DTE , DSNE (Diploma in Special Needs Education) na ECDE (Early Childhood Development) viko tayari kukusanywa.

•KNEC iliagiza walio na maswali wayawasilishe mtandaoni kupitia Mfumo wa Taarifa za Kusimamia Maswali (QMIS)

Image: star

Baraza la Kitaifa la Mitihani la Kenya (KNEC) limeagiza watahiniwa waliofanya mitihani ya viwango mbalimbali katika miaka ya 2022 na 2023 kuchukua vyeti vyao kutoka kwa taasisi zao.

KNEC ilisema vyeti vya KCSE 2022, 2022 na 2023 DTE (Diploma in Teacher Education), DSNE ( Diploma in Special Needs Education) na ECDE (Early Childhood Development) viko tayari kukusanywa.

Zaidi ya hayo, vyeti vya PTE (Primary Teacher Examination), UDPTE (Upgrade Programme for the Diploma in Primary Teacher Education) na UDECTE (Upgrade Programme for the Diploma in Early Childhood Teacher Education) pia vimetumwa.

Bodi ya mitihani ilisema vyeti hivyo vimetumwa kwa shule ambako watahiniwa walifanya mitihani yao.

"Ikiwa umekuwa ukisubiri cheti chako unachostahili, cheti chako kimefika katika taasisi uliyofanya mtihani na iko tayari kuchukuliwa," KNEC ilisema kwenye chapisho kwenye X.

Baraza limewapongeza watahiniwa wote na kuwataka wasichelewe kuchukua vyeti vyao.