Rais Ruto awarai Gen Z kufanya maandamano ya amani

Mitandao ya kijamii inaendelea kushika moto huku vijana wakijiandaa kwa maandamano ya Nane Nane

Muhtasari

•Ruto alisisitiza kujitolea kwa Kenya kwa amani kwenye maandamano na kuonya dhidi ya maandamano yatayosababisha uharibifu wa mali na kupoteza maisha.

 Inspekta Jenerali, Gilbert Masengeli, alitoa tamko mnamo Agosti 6, 2024, akiwataka waandamanaji kuendelea kuwa na amani

Rais William Ruto
Rais Ruto Rais William Ruto
Image: PCS

Rais William Ruto amewaomba Wakenya kuacha kushiriki maandamano yanayoweza kusababisha ghasia na vurugu.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Kaunti ya Embu Jumatano, tarehe 7 Agosti 2024, Ruto alisisitiza kujitolea kwa Kenya kwa amani kwenye maandamano na kuonya dhidi ya maandamano yatayosababisha uharibifu wa mali na kupoteza maisha.

Ruto alisema, "Sisi ni nchi ambayo tunaamini katika amani. Hatutaki machafuko katika taifa letu. Hatutaki maandamano yanayotoa majanga, kuharibu mali, au kupoteza maisha."

Alitaka wenyeji wa Embu kudumisha amani kufuatia maandamano ya Nane Nane yanayopangwa mnamo Alhamisi, tarehe 8 Agosti 2024.

Ruto aliuliza, “Watu wa Embu wanataka amani au wanataka machafuko? Mnataka amani? Hebu nione kwa mikono wale wanaosema wanataka amani katika taifa letu.”

Maandamano ya Nane Nane, ambayo yanaandaliwa hasa kupitia mitandao ya kijamii, inayoendeshwa na vijana ambao wamekasirishwa na uamuzi wa Ruto wa kurejesha wateule kumi kati ya 22 wa Mawaziri aliyetengua awali.

Aidha, vijana hao wamekasirishwa na uamuzi wa Ruto wa kuajiri wanachama wanne wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) katika Baraza lake la Mawaziri mpya.

Mnamo Julai 24, 2024, Ruto alitangaza uteuzi wa viongozi kutoka ODM, ikiwa ni pamoja na aliyekuwa mwenyekiti wa ODM John Mbadi kuwa Waziri wa Hazina, aliyekuwa Kiongozi wa Wachache Bungeni Opiyo Wandayi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, na Manaibu Viongozi wa ODM Wycliffe Oparanya na Hassan Joho kuwa Mawaziri wa Ushirikiano na Madini, mtawalia.

Ruto alielezea uteuzi huu kama sehemu ya juhudi zake za kuunda serikali pana inayojumuisha mitazamo mbalimbali.

Hatua ya Rais, ambayo inalenga kuimarisha umoja wa kitaifa na kushughulikia hisia za upinzani, imezua kutoridhika kwa baadhi ya vijana wa Kenya, ambao wanajiandaa kwa maandamano ya Nane Nane kupitia mitandao ya kijamii.

Katika hatua ya kujibu, Kamishna wa Polisi anayekalia wadhifa wa Inspekta Jenerali, Gilbert Masengeli, alitoa tamko mnamo Agosti 6, 2024, akiwataka waandamanaji kuendelea kuwa na amani na kuonya kuhusu hatua za kisheria kwa wale watakaovunja sheria.

Tamko hilo lilionyesha uwezekano wa kurudi kwa mapigano kati ya polisi na waandamanaji.

Mitandao ya kijamii inaendelea kushika moto huku vijana wakijiandaa kwa maandamano ya Nane Nane, ikionyesha mvutano unaoendelea na machafuko ya kisiasa.