logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC yatangaza maeneo ambayo yatakosa stima leo, Jumapili

Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na  Nairobi, Kisumu, Lamu, na Kisii.

image
na Radio Jambo

Habari25 August 2024 - 05:26

Muhtasari


•Kampuni ya KPLC ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

•Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na  Nairobi, Kisumu, Lamu, na Kisii.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumapili, Agosti 25.  

Katika taarifa ya Jumamosi jioni, kampuni hiyo ilisema kukatizwa kwa umeme kutatokana na ukarabati ambao utakuwa ukifanyiwa kwenye mitambo.

Walisema baadhi ya maeneo ya kaunti nne za Kenya yatakosa umeme kati ya saa moja asubuhi na saa kumi na moja jioni. Kaunti ambazo zitaathirika ni pamoja na  Nairobi, Kisumu, Lamu, na Kisii.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za mtaa wa Babadogo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Pipeline Estate na Police Line katika kaunti ya Kisumu yataathirika kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za mji wa Kisii katika kaunti ya Kisii pia zitakosa umeme kati ya saa moja asubuhi na saa tisa alasiri.

Baadhi ya sehemu za maeneo ya Lamu na Mokowe katika kaunti ya Lamu zitaathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved