logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto awaonya wakuu wa shule wanawaonyanyasa wazazi kuhusu karo

"Tulitoa Sh62 bilioni mnamo Januari kusomesha wanafunzi wetu"

image
na

Habari21 January 2024 - 12:26

Muhtasari


• Ruto aliwasili Teso Jumapili asubuhi kwa mkutano wa maombi ya madhehebu mbalimbali.

• Alisema wizara ya Elimu itafuatilia kwa karibu utendaji kazi katika taasisi ili kuhakikisha wanafunzi wote wanasalia shuleni.

Rais Ruto akiwa BUSIA

Rais William Ruto amewaamuru wakuu wa taasisi kuwaruhusu  wanafunzi kufanya masomo bila kujali kama wamelipa karo au la.

Ruto alisema serikali tayari imetoa pesa kwa ajili ya masomo na ni 'utovu wa maadili' kwa wakuu wa shule kuendelea kuwahangaisha wazazi na wanafunzi kwa kutolipa karo.

"Tulitoa Sh62 bilioni mnamo Januari kusomesha wanafunzi wetu. Lakini hata baada ya maendeleo haya kuna wakuu wa shule wanawaambia wazazi walipe karo kwa sababu serikali haijatoa pesa kwa shule," Ruto alisema.

“Tunajua umuhimu wa elimu na tunataka watoto wetu wote waende shule, wasimamizi wa taasisi waache kutumia fursa ya mazingira magumu ya wananchi wetu kuwalazimisha wazazi kulipa ada ya shule kwa kisingizio kwamba serikali haijatoa fedha.

Ruto aliyasema hayo Jumapili alipowasili katika Shule ya Msingi ya MachakusI kwa mkutano wa maombi ya madhehebu mbalimbali katika kanisa la Machakusi ACK eneo bunge la Teso Kusini, Busia.

Ruto aliwasili Teso Jumapili asubuhi kwa mkutano wa maombi ya madhehebu mbalimbali.

Alisema wizara ya Elimu itafuatilia kwa karibu utendaji kazi katika taasisi ili kuhakikisha wanafunzi wote wanasalia shuleni.

Kamanda mkuu ambaye anazuru Busia kwa mara ya tatu tangu achukue wadhifa huo kutoka kwa mtangulizi wake Uhuru Kenyatta, anaandamana na viongozi wengi kutoka pande zote za mgawanyiko wa kisiasa.

Baada ya maombi hayo, Mkuu wa Nchi amepanga kuzindua rasmi mradi wa maji safi na maji taka wa Malaba-Malakisi unaogharimu mamilioni ya fedha katika eneo la Amoni kabla ya kuhutubia katika mji wa Malaba.

Baadaye, atasafiri hadi Ang’urai ambako atahutubia mkutano mwingine kabla ya kuzuru Shule ya Kitaifa ya Wasichana ya Kolanya, kulingana na Mbunge wa Teso Kaskazini Oku Kanya.

Miongoni mwa viongozi wanaoandamana na Rais ni pamoja na Waziri Mkuu Musalia Mudavadi, Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetangula, Katibu Mkuu wa Utawala katika Ofisi ya Rais Arthur Osiya, Magavana Paul Otuoma (Busia) na Kenneth Lusaka (Bungoma), Waziri wa Michezo Ababu Namwamba, Naibu Waziri wa Michezo. Gavana Arthur Odera na PS Susan Mangeni wa Biashara Ndogo na za Kati.

Wengine ni wabunge Oku Kaunya (Teso Kaskazini), Mary Emase (Teso Kusini), Phelix Odiwuor almaarufu Jalango (Langata) na John Waluke (Sirisia).

Rais Ruto akiwa BUSIA
Rais Ruto akiwa BUSIA
Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved