logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama safari ya mapenzi ya Zari na Shakib, watafanya harusi rasmi Oktoba 3

Walihalalisha muungano wao kwa mara ya kwanza katika harusi ya kidini ya Kiislamu (Nikah) mapema mwaka huu.

image
na Radio Jambo

Habari02 October 2023 - 11:12

Muhtasari


•Zari na mchumba wake Shakib wanatarajiwa kufunga pingu za maisha katika harusi rasmi ya kizungu mnamo Oktoba 3.

•Walihalalisha muungano wao kwa mara ya kwanza katika harusi ya kidini ya Kiislamu (Nikah) mapema mwaka huu.

Wapenzi mashuhuri wa Uganda, Zarinah Hassan na Shakib Cham Lutaaya wanatarajiwa kufunga pingu za maisha katika harusi rasmi ya kizungu hivi karibuni.

Barua ya mwaliko ambayo ilifikia Radio Jambo inaonyesha kuwa harusi hiyo itafanyika Jumanne, Oktoba 3 mwendo wa saa sita adhuhuri.

“Zarinah Hassan na Shakib Lutaaya wanakualika kwa moyo mkunjufu kushiriki katika furaha na kusherehekea siku yao ya harusi. Tarehe: 3 Oktoba 2023. Saa: 1200. Uwepo wako kwenye siku hii maalum utafanya sherehe yetu isisahaulike.” ilisomeka barua ya mwaliko ambayo ilitiwa saini na Zari na Shakib.

Harusi itakayofanyika nchini Afrika Kusini itahudhuriwa na wageni wachache tu ambao wamealikwa na maelezo mengi kuihusu yamewekwa faragha. 

Wawili hao walihalalisha muungano wao wa muda mrefu kwa mara ya kwanza katika harusi ya kidini ya Kiislamu (Nikah) mapema mwaka huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved