logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Walinipa Sh50m kuacha kinyang'anyiro cha Mbunge wa Mathare - Bahati

Mmiliki wa tikiti ya Jubilee alifichua kuwa pia aliahidiwa kazi.

image
na Radio Jambo

Habari29 June 2022 - 14:53

Muhtasari


  • Mmiliki wa tikiti ya Jubilee alifichua kuwa pia aliahidiwa kazi
  • Bahati alisema hawezi kuhujumiwa akidai ndiyo sababu wapinzani wake wamebuni njia nyingine za kumwangusha
Kelvin Bahati Kioko anayelenga ubunge Mathare kupitia chama cha Jubilee

Msanii wa Kenya Kelvin Bahati Kioko anadai alipewa Sh50m kuacha kinyang'anyiro cha ubunge cha Mathare.

Akizungumza na Radio Citizen siku ya Jumatano, Bahati alisema wapinzani wake wamekuwa wakimpigia debe ajiuzulu.

“Wamenipatia mamilioni hadi Sh50 milioni wanajua wakifika ofisini watapata fedha,” alisema.

Mmiliki wa tikiti ya Jubilee alifichua kuwa pia aliahidiwa kazi.

“Lakini sitafuti kazi, najitafutia riziki kutokana na muziki wangu,” alisema.

Bahati alisema hawezi kuhujumiwa akidai ndiyo sababu wapinzani wake wamebuni njia nyingine za kumwangusha.

Alimtaja mbunge aliyeko madarakani Anthony Oluoch kuwa mmoja wa waliofika kwake kuomba uungwaji mkono.

"Aliniambia nimfanyie wimbo wa kampeni na kumuunga mkono. Wanataka kumtumia mtu wa Mathare kufika kwa watu."

Bahati alisema anajuta kwamba katika nyanja ya siasa, mtu hawezi kuwa na marafiki anaoweza kuwaamini.

"Ninakosa marafiki wa kweli, katika siasa, unakaa na rafiki yako ambaye anasema wasichomaanisha. Wanasiasa wengi sio wa kweli."

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved