logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mutahi Ngunyi awashauri Wakenya kumuunga mkono Winnie Odinga na Charlene Ruto

Kulingana na taarifa yake, wanawake bado hawajafikia kile kinachofanyika Ulaya.

image
na Radio Jambo

Habari16 November 2022 - 14:58

Muhtasari


  • Kupitia kwenye akaunti yake ya Twitter alisema kuwa wanawake hao wawili wataenda kukuza nguvu za wasichana humu nchini

Mchanganuzi maarufu wa Kisiasa Mutahi Ngunyi amewashauri Wakenya kuwaunga mkono Winnie Odinga na Charline Ruto.

Kupitia kwenye akaunti yake ya Twitter alisema kuwa wanawake hao wawili wataenda kukuza nguvu za wasichana humu nchini.

Kulingana na taarifa yake, wanawake bado hawajafikia kile kinachofanyika Ulaya.

Aliunga mkono hilo zaidi kwa kuongeza kuwa Mawaziri Wakuu wanawake katika nchi za Ulaya hata wananyonyesha kwenye sakafu ya mabunge.

Hii inaonyesha wamejitwika jukumu la kutawala baada ya kupata uungwaji mkono wa hali ya juu kutoka kwa wananchi.

Kauli yake inajiri baada ya baadhi ya watu kukosoa uteuzi wa Winnie Odinga kwa EALA.

Aliteuliwa na muungano wa Azimio pamoja na mwanawe Kalonzo. Baadhi pia wamemtetea wakisema kuwa jina la babake halimfafanui kwa vile ana uwezo.

Kwa upande mwingine, Charlene Ruto hajateuliwa katika kiti chochote lakini hivi majuzi, amekuwa akionyesha nia ya ulimwengu wa siasa.

Ameonekana akihudhuria mikutano na viongozi hapa nchini Kenya na nje.

Ndugu wabunge Muunge mkono Winnie Odinga. Yeye ndiye maisha ya SIASA zetu na Charlene Ruto.Nguvu ya Msichana lazima Itawale. Huko Ulaya, Mawaziri Wakuu Wanawake wananyonyesha kwenye sakafu ya Bunge,"Mutahi alisema.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved