logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Karibu nidhani ni Chebukati!" Wanatwitter wamtania Kabogo kwa upara wake

Safari hii alikuwa bila kofia katika mazishi ya dadake Moses Kuria.

image
na Radio Jambo

Makala24 January 2023 - 10:01

Muhtasari


• Kabogo alikuwa katika mazishi ya dadake Moses Kuria akiwa bila kofia.

• Hapo ndio wengi walipata fursa ya kuona kile ambacho amekuwa akificha kwenye kofia kwa muda mrefu.

William Kabogo ataniwa upara kama wa Chebukati

Jumatatu, aliyekuwa gavana wa kwanza wa Kiambu William Kabogo alipakia rundo la picha akiwa amehudhuria hafla ya mazishi ya dadake waziri wa biashara na viwanda Moses Kuria, Pauline Nyokabi Kuria katika kaunti hiyo ya Kiambu.

Kabogo aliungana na rais William Ruto, naibu wake Rigathi Gachagua miongoni mwa watu wengine wengi katika kumuaga dadake waziri Kuria.

“Nilijiunga na Rais H.E. Dk. @WilliamsRuto, naibu wake H.E Riggy G @rigathi na Viongozi wengine wakati wa mazishi ya Pauline Nyokabi Kuria, dada mkubwa wa Waziri wa Biashara, Uwekezaji na Viwanda Mhe. @HonMoses_Kuria katika eneo la Wamwangi katika eneo bunge la Gatundu Kusini. Mei Yeye R.i.P,” Kabogo aliandika.

Hata hivyo, gumzo kubwa halikuwa katika Kabogo kuhudhuria hafla ya mazishi, bali ni katika muonekano wake.

Kwa muda mrefu Kabogo amekuwa akionekana na kofia kichwani lakini safari hii alikuwa kichwa tupu bila kofia, jambo ambalo lilivutia maoni mengi ya utani kwenye Twitter.

Wengi walimtania kuhusu upara wake ambao ulikuwa umeangaza kweli kweli katikati ya nywele zake huku wakifananisha kichwa chake na kile cha aliyekuwa mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC, Wafula Chebukati.

Wengine walidhani kuwa hicho si kipara bali ni njia mpya ambayo mkwasi huyo wa Kiambu amekuja nayo ya kunyoa mwaka 2023.

“Kuuliza tu, hicho ni kipara ama ni staili mpya ya kunyoa mwaka mpya 2023?” mmoja kwa jina Lewis alimuuliza.

“Una hairstyle mpya, au "uwanja wa ndege" imekuwa huko wakati wote? Hutambulikani, Mhesh!” mwingine alimtania.

“Karibu nikuchanganye na Chebukati kwa hicho kichwa chako mheshimiwa,” Collins Cheruiyot alisema.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved