logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge Babu Owino na mbunge Peter Salasya walimana mitandaoni

Mbunge  Babu Owino, ameorodheshwa mbunge wa pili bora nchini akipewa asilimia 72.1.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 May 2023 - 12:29

Muhtasari


  • Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro aliorodheshwa kidedea – bora zaidi kwa asilimia 73.7 kulingana na ripoti ya Politrack Africa, huku Patrick Makau (Machakos) akiwa wa tatu (70.6).

Vita vya maneno kati ya mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino na mwenzake wa Mumias Mashariki, Peter Salasya vimeshuhudiwa mitandaoni kufuatia ripoti ya hivi punde ya rekodi ya utendakazi.

Vita hivyo vimeibuka  kutokana na ripoti hiyo, inayomuorodhesha Babu Owino kama mmoja wa wabunge wanaoongoza katika utendakazi wa maeneobunge nchini.

Huku akiikosoa ripoti hiyo ya Politrack Africa, Salasya amedai imefadhiliwa na Babu Owino.

Salasya, anayehudumu kipindi cha kwanza bungeni anaamini anafanya bora zaidi.

Akiandka na kutoa madai hayo kupiria kwenye akaunti yake rasmi ya twitter mbnge huyo alisema;

“Ripoti ya Politrack Africa ni uongo mtupu, hata katika Twitter akaunti yangu ina wafuasi wengi kuliko yao. Mfadhili wao ni Babu Owino, ambaye ni miongoni mwa wafuasi wachache wanaowafuata. Mara hii tumewashika,” Salasya alisema.

“Ninaamini nimefanya kazi bora nyanjani na ninakua kisiasa, na hata wao wanajua hivyo ndio maana wananunua kampuni kutoa ripoti ghushi ya utendakazi kujaribu kunitisha. Nina malengo makuu."

Mbunge  Babu Owino, ameorodheshwa mbunge wa pili bora nchini akipewa asilimia 72.1.

Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro aliorodheshwa kidedea – bora zaidi kwa asilimia 73.7 kulingana na ripoti ya Politrack Africa, huku Patrick Makau (Machakos) akiwa wa tatu (70.6).

Akimjibu Salasya, Babu Owino aliandika katika ukurasa wake rasmi wa twitter: “Mheshimiwa Peter Kalerwa Salasya, Politrack iliorodhesha wabunge kwa mujibu wa utendakazi wao ila sio kwa uwendawazimu. Ulichaguliwa kufanyia wananchi kazi, ila si kuwa mcheshi wa kijijini na mwendawazimu…”

 

Mbunge huyo wa chama cha ODM, pia anaongoza katika orodha ya wabunge kiwango cha kaunti, Nairobi.

Licha ya maneno makali ambayo wawili hao wamerushiana,bila shaka wabunge hao ni wafuasi sugu wa kinara wa ODM Raila Odinga.

Pia walionekana wakiwa mstari wa mbele katika maandamano wa Azimio ya kupinga Serikali kuu wiki zilizopita

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved