logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wacha kuhujumu Kenya Kwanza furahia kustaafu kwako-Millient Omanga kwa Uhuru

Alikuwa akizungumza wakati wa mazishi ya aliyekuwa mke wa Waziri wa zamani Amos Kimunya

image

Habari20 February 2024 - 14:06

Muhtasari


  • Uhuru Jumamosi aliikashifu serikali ya Kenya Kwanza akisema viongozi waliochaguliwa afisini wanapaswa kuzingatia mbele na kukoma kutazama yaliyopita.
Seneta mteule Millicent Omanga

Aliyekuwa Seneta mteule Millicent Omanga amemtaka Rais wa zamani Uhuru Kenyatta kuachana na masuala ya serikali ya Kenya Kwanza.

Omanga, mshirika wa Rais William Ruto, alisema Jumanne rais huyo wa zamani anafaa kuiga watangulizi wake na kufurahia kimyakimya kustaafu kwake.

“Rais wa zamani Uhuru Kenyatta angejifanyia upendeleo mkubwa kwa kufurahia kustaafu kwake bila kuonekana kuhujumu utawala wa Kenya Kwanza. Wacha aige watangulizi wake, "alisema katika taarifa kwenye mtandao wa X.

Uhuru Jumamosi aliikashifu serikali ya Kenya Kwanza akisema viongozi waliochaguliwa afisini wanapaswa kuzingatia mbele na kukoma kutazama yaliyopita.

Alikuwa akizungumza wakati wa mazishi ya aliyekuwa mke wa Waziri wa zamani Amos Kimunya, Lucy Wanjiru, katika Shule ya Foothills, Kipipiri katika Kaunti ya Nyandarua.

"Kama wewe ni kiongozi wa maana, kiongozi wa maana anashika usukani anaangalia mbele, sio kila saa kunagalia rear view ati ametoka wapi," alisema.

Uongozi mkuu wa Kenya Kwanza ulijibu vivyo hivyo huku Ruto na Naibu Rais Rigathi Gachagua wakitetea mtindo wao wa uongozi.

Wawili hao baada ya muda wamelaumu utawala wa Jubilee kwa maelfu ya makosa ikiwa ni pamoja na kukopa kupita kiasi na ruzuku isiyo ya lazima ambayo wanasema kwa sehemu ilichangia gharama ya juu ya maisha ya sasa.

“Kama unataka kuongoza nchi, angalia mbele. Usizingatie maongezi na mchezo wa lawama bila sababu,” Uhuru aliongeza kwa lugha yake ya asili ya Kikuyu.

 

“Hakuna pahali mnaenda, hakuna pahali mnapeleke nchi. Nchi inataka viongozi wako na maono ya mbele kwa sababu hiyo ndiyo itakuwa ya manufaa, kutatua shida zile zako nazo,” aliongeza.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved