Waziri aliyefutwa hatimaye amtumia salamu mwanahabari maarufu baada ya kutopatikana miezi 20

James Smart alibainisha kuwa waziri huyo ambaye inaonekana hajateuliwa tena kwenye baraza la mawaziri alimsalimia.

Muhtasari

•James Smart amemfichua waziri wa zamani ambaye sasa amemtafuta baada ya kutimuliwa kwenye baraza la mawaziri.

•Waziri huyo hajakuwa akipatikana kwa maoni ya vyombo vya habari katika miezi 20 iliyopita hatimaye alimtumia ujumbe wa salamu.

Image: FACEBOOK/ JAMES SMART

Mwanahabari mashuhuri wa NTV, James Smart amemfichua waziri wa zamani ambaye sasa amemtafuta baada ya kutimuliwa kwenye baraza la mawaziri.

Katika tweet ya Ijumaa asubuhi, msomaji huyo wa habari alifichua kwamba waziri huyo ambaye hajakuwa akipatikana kwa maoni ya vyombo vya habari katika miezi ishirini iliyopita hatimaye alimtumia ujumbe wa salamu.

Smart alibainisha kuwa waziri huyo ambaye inaonekana hajateuliwa tena kwenye baraza la mawaziri alimsalimia, na akadokeza kuwa hatamjibu.

"Nilipokea "Habari kaka" ya kwanza kutoka kwa waziri wa zamani na ambaye sasa amefukuzwa kazi. Hajapatikana kwa maoni ya vyombo vya habari katika miezi 20 iliyopita. Namtakia heri katika ulimwengu wa "Habari", James Smart aliandika Ijumaa asubuhi.

Hata hivyo hakutaja jina la waziri anayemzungumzia.

Mnamo Julai 11, Rais Ruto aliwafuta kazi Mawaziri wote na Mwanasheria Mkuu Justin Muturi kama jibu la maandamano ya vijana dhidi ya serikali. Ni naibu wa rais Rigathi Gachagua na Mkuu wa Mawaziri Musalia Mudavadi, ambaye pia ni Waziri wa Masuala ya Kigeni pekee ndiye aliyesalimika.

Rais kufikia sasa amewateua mawaziri wapya kujenga baraza lake jipya la mawaziri na kuwateua tena baadhi ya mawaziri ambao alikuwa amewafuta kazi.

Ruto hata hivyo aliwaacha nje Moses Kuria ambaye alikuwa Waziri wa Utumishi wa Umma na Peninah Malonza ambaye alikuwa waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Wengine ambao hawakutajwa katika kundi la pili ni pamoja na Aisha Jumwa ambaye alikuwa waziri wa Jinsia na Utamaduni na aliyekuwa Waziri wa Hazina ya Kitaifa, Njuguna Ndung'u.

Zacharia Njeru ambaye alihudumu kama Waziri wa Maji na Umwagiliaji aliachwa nje na Mithika Linturi (Kilimo na Mifugo), Ezekiel Machogu(Elimu), Ababu Namwamba(Michezo) na Simon Chelugui(Biashara Ndogo kiasi na Ndogo).

Florance Bore ambaye alikuwa hadi kufukuzwa kwake Waziri wa Kazi na Ulinzi wa Jamii aliachwa nje pamoja na Eliud Owalo(ICT) na Susan Nakhumicha(Afya).