logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kostany na Sudi wamsuta rais Uhuru kwa kumshambulia DP Ruto hadharani

Sudi amesema wawili hao watasalia serikalini   licha ya kuwepo tofauti kati yao hadi  wakenya wapige kura kuamua atakayechukua usikani wa nchi mwaka ujao .

image
na Radio Jambo

Makala14 February 2021 - 17:42

Muhtasari


  •  Sudi amesema wawili hao watasalia serikalini   licha ya kuwepo tofauti kati yao hadi  wakenya wapige kura kuamua atakayechukua usikani wa nchi mwaka ujao .
  •  Wabunge Caleb Kostany na Oscar Sudi s wamesema rais hana mamlaka  ya kumfuta kazi naibu wake  na mashambulizi hayo dhidi ya Ruto hayafai  kwani naibu wake hajamkosea heshima .

Washirika wa naibu wa rais William Ruto kutoka Rift Valley wamemkosoa vikali rais Uhuru Kenyatta kwa kumshambulia Ruto hadharani baada ya Kenyatta kumtaka Ruto ajiuzulu kutoka serikalini badala ya kuihujumu akiwa ndani .

 Wabunge Caleb Kostany na Oscar Sudi s wamesema rais hana mamlaka  ya kumfuta kazi naibu wake  na mashambulizi hayo dhidi ya Ruto hayafai  kwani naibu wake hajamkosea heshima .

 Sudi amesema wawili hao watasalia serikalini   licha ya kuwepo tofauti kati yao hadi  wakenya wapige kura kuamua atakayechukua usikani wa  nchi  mwaka ujao .

 Ijumaa iliyopita rais Uhuru Kenyatta alionekana kumshambulia naibu wake kwa kumtaka ajizulu kutoka serikali badala ya kuikosoa na wakati mwingine kujisifia  baadhi ya mafanikio ya serikali  ambayo bado anaikosoa . Ruto kwa upande wake alisema hajamkosea heshima rais na ataendelea kuhudumu katika wadhifa wake kwani nafasi yake imelindwa na katiba licha ya kuwa majukumu yake yamekabidhiwa watu wengine . Ruto ameendelea na kampeini za kujipigia debe ili kumrithi rais Uhuru ambaye ameonekana kubadilisha msimamo wake  kuhusu kumuunga mkono   katika uchaguzi wa 2022 ili achukue usukani wakati muhula wake wa pili utakapotamatika .

 Tofauti kati ya viongozi hao wawili wa Jubilee imezidishwa na misimamo yao tofauti kuhusu   Ripoti ya BBI ambayo ais anaiunga mkono akiwa  na mshirika wake mpya wa kisiasa Raila Odinga lakini inapingwa vikali na Ruto anayeshikilia kwamba katiba  ya mwaka wa 2010 haifai kurekebishwa . Ruto na washirika wake wanahisi kwamba marekebisho hayo ya katiba yanalenga kumzuia kuchukua hatamu za uongozi kutoka kwa Uhuru ambaye alikuwa ameahidi kumpiga jeki Ruto ahudumu kipindi cha miaka 10 kama rais .

  


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved