logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ajali! kaunti ya kilifi yaomboleza vifo vya wafanyikazi sita

Ajali! kaunti ya kilifi yaomboleza vifo vya wafanyikazi sita

image
na Radio Jambo

Habari08 April 2021 - 07:49

Muhtasari


• Gavana Amason Kingi alithibitisha kupoteza wafanyikazi wake  akisema wengi waliofariki ni wa idara ya ukusanyaji pesa.

• Ajali hiyo  ilihusisha basi la kampuni ya Muhsin Bus  na basi la kampuni ya Sabaki Shuttle.

Serikali ya kaunti ya Kilifi inaomboleza vifo vya wafanyikazi wake sita.

Sita hao walikuwa miongoni mwa watu 15 waliofariki katika ajali mbaya ya barabarani siku ya Jumatano katika eneo la Kwamkikuyu kwenye barabara kuu ya Malindi Mombasa.

Maafisa wa kaunti sita pamoja na wengine ambao walinusurika walikuwa safarini wakielekea kazini na walikuwa wameabiri basi ya kampuni ya Sabaki kutoka eneo la Marereni ajali hiyo ilipotokea.

 

Gavana wa Kilifi Amason Kingi alithibitisha kupoteza wafanyikazi wake.

“kwa kawaida wao hutumia basi ndogo kusafiri kutoka Malindi ambapo wanakaa hadi Kilifi wanako fanyia kazi,” Kigi alisema alipozuru eneo la ajali.

Alisema wengi waliofariki ni wa idara ya ukusanyaji pesa.

Ajali hiyo ilitokea katika eneo la Kwamkikuyu na ilihusisha basi la kampuni ya Muhsin Bus lililokuwa safarini kwenda Garissa kutoka Mombasa na basi la kampuni ya Sabaki Shuttle lililokuwa likielekea Merereni.

Madereva wote wawili walifariki papo hapo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved