logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Spiderman' akamatwa mjini Nairobi kuhusiana na wizi

'Spiderman' akamatwa mjini Nairobi kuhusiana na wizi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri12 April 2021 - 07:17

Muhtasari


• Mshukiwa huyo ambaye alibandikwa jina "Spiderman 3" alitambuliwa kama Kennedy Otieno Oyier.

• Jambazi huyo  amekuwa akikwea kuta katika mitaa mbali mbali mjini  Nairobi na kuiba vifaa vya elektroniki, pesa na vito vya mapambo.

Mshukiwa baada ya kukamatwa

Jambazi ambaye amekuwa akikwea kuta katika mitaa mbali mbali mjini  Nairobi na kuiba vifaa vya elektroniki, pesa na vito vya mapambo amekamatwa.

Mshukiwa huyo ambaye alibandikwa jina "Spiderman 3" alitambuliwa kama Kennedy Otieno Oyier.

Kennedy ni ndugu wa mtuhumiwa mwingine - John Otieno Oyier- ambaye alikuwa amekamatwa mwezi Januari mwaka huu na kushtakiwa kortini kuhusu wizi na kuzuiliwa katika gereza la Viwandani, polisi walisema siku ya Jumatatu.

Kennedy alikamatwa siku Jumapili usiku katika operesheni kufuatia kuongezeka kwa visa vya wizi katika mitaa ya Kileleshwa, Parklands, Lavington, Muthangari na Westlands.

Amekuwa mafichoni baada ya kujua kwamba alikuwa kisakwa na maafisa wa polisi kwa siku kadhaa zilizopita Alikuwa akikimbia katika wiki zilizopita.

Alikuwa amebadilisha makazi yake baada ya kaka yake kukamatwa.

Kennedy aliwaambia polisi yeye na kaka yake walipata ustadi wa kukwea kuta kutoka kwa sinema ambayo walitazama mtandaoni.

Alisema wamefika kwenye makazi mengi katika maeneo hayo na kufanikiwa kuiba vitu vya thamani baada ya kuvunja nyumba kwa kutumia chuma na funguo.

Wanafanya hivyo wakikwepa mahali ambapo kuna taa au kamera.

Wanafanya hivyo mwishoni mwa wiki, asubuhi na mapema au wakati wa usiku wakati wenyeji hawako.

Baada ya kukamatwa, mshukiwa huyo aliwaongoza maafisa kwenda kwenye makazi yake huko Kawangware ambapo mabegi kadhaa ya laptop yalipatikana na magari mawili ambayo yalibururwa hadi Kituo cha Polisi cha Kilimani.

Polisi wanataka wale walioathiriwa kuzuru kituo hicho kufanikisha upelelezi.

Kukamatwa kulifuata msururu wa visa katika maeneo ambayo wakaazi walipoteza vitu vyao vya thamani na pesa.

Polisi wanaamini amekuwa akifanya kazi na walinzi wa nyumba ili kufanikisha wizi wake.

Afisa mkuu wa pilisi wa Nairobi Augustine Nthumbi alisema wanachunguza ili kubaini ikiwa mshukiwa anahusishwa na visa vingine vingi ambavyo vimeripotiwa katika maeneo mengine.

"Tunatafuta washukiwa zaidi ambao tunaamini walikuwa katika sakata hiyo," alisema.

Mshukiwa alikamatwa kwa kosa la wizi na anatarajiwa kortini leo Jumatatu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved