logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Israeli yalipua mnara unazo ofisi za Al jazeera Gaza

Israeli ilikuwa imepeana onyo kuwa ingelipua mnara wa Al Jalaa ulikuwa na makao ya shirika la kijeshi la Hamas na ofisi za nyumba nyingi za Habari za kimataifa ikiwemo Al Jazeera.

image
na Radio Jambo

Habari15 May 2021 - 13:36

Muhtasari


•Wanajeshi wa Israeli walikuwa wamepeana onyo

•Mnara wa Al Jalaa ulikuwa unatumika na kikundi cha Hamas kutekeleza shughuli za kejeshi

Mashambulizi ya mnara wa Al Jalaa

Wanajeshi wa Isreali wamelishambulia kwa bomu na kubomoa mnara wa Al Jalaa ambao una maofisi ya nyumba za habari za kimataifa ikiwemo Al Jazeera na zingine.

Mnara huo ambao pia unatumika kuhifadhi mali ya  kijeshi ya shirika la Hamas limelipuliwa muda mfupi baada ya kutoa onyo kuwa wangelipua  mnara huo.

Hamas ambacho ni kikundi cha kijeshi tokea Palestina kinatawala Gaza kimekuwa lengo la wanajeshi hao wa Israeli kwa muda.

Kupitia akaunti yao ya Twitter, wanajeshi wa Israeli wamesema kuwa shirika la Hamas limekuwa likitumia makazi ya watu kwa shughuli za kijeshi kama kukusanya habari, kupanga shambulio,kutoa amri kudhibiti nakuwasiliana.

“Hamas wakitumia minara kutekeleza shughuli za kijeshoi basi  ni kinyume na sheria na mnara huo unakuwa lengo la shambulio la wanajeshi.” Israeli imetangaza.

Wanajeshi hao wametangaza kuwa wamekuwa wakilipua majumba kama hayo ila wanawapatia watu ilani ya kuhama kabla ya kutekeleza shambulio.

“Majumba yote tuliyobomoa yamekuwa yakitumia kwa shughuli za kijeshi.” Wanajeshi hao wamedai.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved