logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wakati wa mabadiliko uongozini wa Jubilee umefika" Kinyajui

Gavana Lee Kinyajui azungumzia masikitito yake kutokana na masaibu yanayoendelea kukumba chama cha Jubilee

image
na Radio Jambo

Makala20 May 2021 - 19:52

Muhtasari


•Gavana Lee Kinyajui azungumzia masikitito yake kutokana na masaibu yanayoendelea kukumba chama cha Jubilee

•Amekashifu kitendo cha kuwateua wagombeaji kutokana na uhusiano au kuzingatia hisia ama mapato ya kiuchumi.

lee kinyajui

Gavana wa kaunti ya Nakuru, Lee Kinyajui ameeleza masikitito yake kutokana na masaibu yanayoendelea kukumba chama cha Jubilee.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Facebook, Kinyajui ameeleza kuwa wananchi wamekuwa wakinyimwa shaki za kidemokrasia kwenye uteuzi wa wagombeaji viti kwa tikiti ya Jubilee na hilo kusababisha wao kulipiza kisasi kwa kutowachagua wanaoteuliwa.

“Kwenye uchaguzi ndogo zilizofanyika hivi majuzi, ahadi yetu ya kushikilia matakwa ya wananchi na heshima ya haki za kidemokrasia katika uteuzi wa wagombeaji zimekiukwa na hilo limesababisha kuteuliwa kwa wagombeaji wasio na umaarufu” Kinyajui ameeleza.

Kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika katika maeneo ya Juja, Bonchari na Rurii siku ya Jumanne, chama cha Jubilee hakikupata ushindi wowote licha ya kuwa na wagombea viti katika kila eneo. Jambo ambalo limeibua gumzo sana ikikisiwa kuwa huenda chama hicho kimepoteza umaarufu wake.

Kinyajui amesisitiza kuwa ni sharti mabadiliko yafanyike katika uongozi wa chama cha Jubilee huku akisema kuwa chama hicho kimejazwa na watu wengi ambao hawaongezei thamana yoyote kwenye chama.

“Tunaamini wakati wa kutekeleza mabadiliko katika uongozi wa chama umefika. Yafaa tuingize wau wapya ili tufufue ndoto za kuungwa mkono kwa chama” Kinyajui alisema.

Gavana huyo amekashifu kitendo cha kuwateua wagombeaji kutokana na uhusiano au kuzingatia hisia ama mapato ya kiuchumi huku akisema kuwa hiyo ni sawa na kujichimbia kaburi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved