SIASA ZA MT KENYA

Spika Justin Muturi kukamilisha kipindi cha usafisho Ijumaa

Muturi amekuwa katika kipindi cha siku nane za kujitenga kwa minajili ya utakaso kabla ya kutawazwa kuwa msemaji wa eneo la Mt Kenya.

Muhtasari

•Ibada ya kutawazwa itafanyika Mukurwe Wa Nyagathanga siku ya Jumamosi

•Muturi alitarajiwa kutotoka kwenye makazi yake, kutumbuiza wageni, kula aina Fulani ya vyakula ama kushiriki tendo la mapenzi.

Justin Muturi
Justin Muturi

Spika wa bunge la kitaifa, Justin Muturi amekuwa katika kipindi cha siku nane za kujitenga kwa minajili ya utakaso kabla ya kutawazwa kuwa msemaji wa eneo la Mt Kenya.

Akizungumza na wahabari siku ya Alhamisi, Muturi alisema kuwa amekuwa akizingatia mikakati yote aliyoarifiwa na wazee. Hata hivyo, alidinda kutaja aliyofaa kuzingatia huku akisema hilo si jukumu lake

Muturi alizungumzia swala hilo kwa mara ya kwanza tangu kuanza ibada hiyo ya kujitenga akiwa kwenye makao yake  ya Muthaiga huku ameandamwa na wazee.

“Ni kipindi cha tafakari ya kibinafsi ukiwa umeketi, unaenda huko chini kwa mto unangazia vipindi za tafakari ya kibinafsi na kuangazi maneno yanayohusu nchi yetu na eneo letu la Mt Kenya” Muturi alisema.

Spika Mutuki atakamilisha kipindi cha usafisho siku ya Ijumaa kabla ya ibada ya kutawazwa itakayofanyika  katika hekalu ya Mukurwe Wa Nyagathanga iliyoko Murang’a siku ya Jumamosi.

Wazee waliomuandama walieleza kuwa  Muturi alikuwa anapewa Baraka ili aweze kuwapa ushauri

Tunatarajia kupata zaidi ya wazee elfu moja toka pande zote za eneo la Mt Kenay kuhudhuria ibada ya kesho.” Mmoja wa wazee hao aliyetambulishwa kama Peter Kagwanja alitangaza.

Kwa kipindi hicho, Muturi alitarajiwa kutotoka kwenye makazi yake, kutumbuiza wageni, kula aina Fulani ya vyakula ama kushiriki tendo la mapenzi.