•Alikuwa akiosha pikipiki yake kwenye kidimbwi kidogo cha maji kando ya barabara bila kujua kuwa kuna waya ya stima iliyokuwa imeanguka hapo
•Wakenya wamesuta kampuni ya KPLC kwa kutokuwa makini kazini
Kijana mmoja mwendeshaji wa bodaboda upande wa Kanduyi aliuliwa na nguvu za umeme katika kando ya barabara ya Kanduyi-Malaba mapema wiki hii.
Inadaiwa kuwa kijana huyo alikuwa ameenda kuosha pikipiki yake mahala ambapo palikuwa pamekusanyika maji ya mvua bila kujua kuwa kuna waya ya stima iliyokuwa kwenye maji hayo.
Kampuni ya umeme nchini Kenya(KPLC) imetangaza kuwa inatambua kuhusu mkasa huo na inashirikiana na polisi katika kufanya uchunguzi .
“Tunasikitishwa na tukio hilo na tumejitolea kabisa kuhakikisha kuwa suluhisho linapatikana” shirika la KPLC liliandika.
We are aware of the unfortunate electrocution incident which took place at Makutano junction, Kanduyi.
— The Kenya Power & Lighting Company Plc. (@KenyaPower) May 19, 2021
We are co-operating with the police who have commenced investigations into this incident. 1/2
Baadhi ya Wakenya mtandaoni wamesuta kampuni ya KPLC kwa kukosa uwajibikaji na kutojali maslahi ya wanamchi. Pata hapa baadhi ya hisia za Wakenya.
This young man (boda rider) here went to wash his bike as usual along Kanduyi-Malaba road not knowing the kplc cable on the ground was live. He was electrocuted. @RobertAlai @CisNyakundi @NPSOfficial_KE @GovWWangamati @KPLC pic.twitter.com/UByCctLU8p
— Kris Hondoo 🇰🇪 (@KrisHondoo) May 19, 2021
Mkaazi mmoja wa eneo hilo amearifu Radio Jambo kuwa huo sio mkasa wa kwanza wa aina hiyo kutokea upande huo.