logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kangata akashifu serikali ya kaunti kwa kusitisha kambi za matibabu

Serikali ya kaunti ya Muranga imemuagiza seneta Kangata kusitisha huduma za kambi za matibabu kutokana na janga la COVID 19

image
na Radio Jambo

Habari22 May 2021 - 09:25

Muhtasari


•Serikali ya kaunti ya Muranga imemuagiza seneta Kangata kusitisha huduma za kambi za matibabu kutokana na janga la COVID 19

Kangata

Seneta wa Murang’a, Irungu Kang’ata amekashifu kitendo cha serikali ya kaunti kujaribu kusitisha kambi zake za matibu.

Kupitia ujumbe aliochapisha kwenye ukurasa wake wa Twitter, Kangata ametaja tendo hilo kuwa haramu;.

“Nia ya serikali ya kaunti ya Murang’a kusitisha kambi zangu za matibabu ni haramu. Hii ni kukiuka haki za wagonjwa wanyonge kwa kuwanyima matibabu bure ya hali ya juu yanayosaidia yale ya hospitali za kaunti” Kang’ata aliandika.

Kangata alikuwa anasema haya kutokana na barua ya kusitisha huduma hizo aliyopokea siku ya Alhamisi kutoka kwa waziri wa afya katika kaunti ya Muranga, Joseph Mbai.

Kwa upande wa serikali ya kaunti hiyo, Mbai alieleza kuwa huduma zile zilikuwa zimesitishwa kutokana na janga la COVID 19.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved