logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aisha Jumwa akanusha madai kuwa bintiye alijitia kitanzi

Ilidaiwa kuwa bintiye Jumwa alijitia kitanzi akiwa katika shule ya upili ya Kalimoni na mwili wake kupatikana kwenye ukumbi wa kulia

image
na Radio Jambo

Yanayojiri23 May 2021 - 06:21

Muhtasari


“Sisi sote ni wazima, msichana wangu ni mzima na tunamshukuru Mungu kwa ajili ya afya yake. Hizi zinazotembea katika mitandao ni propaganda tu” Jumwa alisema.

Aisha Jumwa

Mbunge wa Malindi, Bi Aisha Jumwa amekanusha madai kuwa bintiye alijiua kwa kujitia kitanzi akiwa shuleni.

Jumwa amewataka Wakenya kutupilia mbali madai hayo huku akiwaagiza wanamitandao kuepuka kueneza propaganda kutokana na uvumi usio na msingi.

Jumwa alikuwa akizungumza akiwa katika eneo bunge lake siku ya Jumamosi.

“Sisi wote ni wazima, msichana wangu ni mzima na tunamshukuru Mungu kwa ajili ya afya yake. Hizi zinazotembea katika mitandao ni propaganda tu” Jumwa alisema.

Ilidaiwa kuwa mwanawe Jumwa, Melisa Katana alijitia kitanzi akiwa katika shule ya upili ya Kalimoni na mwili wake kupatikana kwenye ukumbi wa kulia. Picha ya msichana aliyemfanana sana mbunge huyo iliwekwa chini ya ripoti hizo zilizosambazwa mtandaoni jambo ambalo ripoti hiyo kuaminika.

Hata hivyo, ripoti zinaarifu kuwa tukio hilo lilifanyika nchini Ghana ila si bintiye Jumwa kama ilivyodaiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved