logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chama cha Jubilee chamteua Njama kupeperusha bendera Kiambaa

Kariri Njama atapambana na Raymond Kuria wa PEP, John Njuguna wa UDA kati ya wengine

image
na Radio Jambo

Yanayojiri22 May 2021 - 19:50

Muhtasari


•Uteuzi wa wagombeaji ulifanyika kwa njia ya mahojiano ya moja kwa moja

•Wagombeaji watano walihojiwa

Kariri Njama

Chama tawala cha Jubilee kimemteua Kariri Njama kupeperusha bendera kwenye uchaguzi mdogo katika eneo bunge la Kiambaa.

Njama ameteuliwa baada ya kuibuka mshindi wa mahojiano yaliyofanyika katika ofisi za Jubilee zilizoko Pangani siku ya Jumamosi.

Mahojiano hayo yalishirikisha wagombeaji watano ikiwemo Josphat Gichuhi, Lenah Koinange, June Koinange, Damaris Wambui na Njama ambaye aliibuka wa kwanza akifuatwa na Damaris. Wafuasi wa wagombeaji hao waliwaandama na kungoja matokeo nje ya ofisi za Jubilee.

Katibu Mkuu wa chama hicho cha Jubilee alihakikishia wafuasi wa wagombeaji hao kuwa shughuli ile ilifanywa kwa haki.

Njama atamenyana na Raymond Kuria wa People Empowerment Party(PEP) na John Njuguna Wanjiku wa United Democratic Party (PEP) kati ya wengine katika uchaguzi utakaofanyika tarehe 15 Julai.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved