•Atwoli amekanusha madai kuwa bango hilo limeng'olewa huku akiagiza wanaoeneza uvumi huo kuacha kupoteza wakati wao.
•Atwoli pia alimkashifu vikali wakili tajika Ahmednasir Abdullahi almaarufu kama Grand Mulla kwa kusema kuwa kupatia barabara jina la Atwoli ni aibu kubwa.
Serikali ya kaunti ya Naorobi ilibadilisha jina la barabara ya Dik Dik iliyo eneo la Kileleshwa na kuipa jina mpya 'Francis Atwoli Road' siku ya Alhamisi.
Katibu mkuu wa COTU alipongeza serikali hiyo kwa kile alichoita kuheshimu wafanyikazi wote na viongozi wa miungano ya wafanyikazi walioaga. Hata hivyo, uzinduzi wa barabara hiyo haukupokelewa kwa furaha na maelfu ya Wakenya mitandaoni huku wakikashifu na kukejeli hatua hiyo.
Baadhi ya wanamitandao walikuwa wametishia kung'oa bango lililoonyesha jina mpya ya barabara hiyo huku picha ya bango lile likiwa imebebwa na lori ikisambazwa mitandaoni ikisemekana kuwa lilikuwa limengolewa na wananchi wenye ghadhabu punde baada ya kuwekwa.
Atwoli amekanusha madai kuwa bango hilo limeng'olewa huku akiagiza wanaoeneza uvumi huo kuacha kupoteza wakati wao. Radio Jambo pia imethibitisha kuwa bango hilo bado limo. Picha inayozunguka mitandaoni ikionyesha bango hilo likiwa kwa lori imeripotiwa kupigwa wakati bango hilo lilikuwa linapelekwa kuwekwa pale.
"Hakuna kilichotolewa ili kuwafanya mfurahie, msipoteze muda mkisherehekea habari za uongo! Mapenzi ya Mungu ni makuu." Atwoli aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Nothing was removed to make you happy, don’t waste your time celebrating fake news !God’s wish is Paramount.
— Francis Atwoli NOM (DZA), CBS, EBS, MBS. (@AtwoliDza) May 28, 2021
Kwa ujumbe mwingine kupitia akaunti ya COTU, muungano huo ulidai kuwa uvumi huo ulikuwa unaenezwa na mlengo wa kisiasa wa naibu rais almaarufu kama 'Hustler Nation'
"Wanachukia kazi kubwa na mafanikio ambayo ni ya kusifiwa . Katibu mkuu wa COTU amejitolea kuhudumia wafanyakazi wa Kenya, Afrika na dunia bila ubinafsi na jambo hilo limepokelewa na serikali ya Kaunti ya Nairobi." muungano huo ulisema.
Fake News from "Hustler Nation Press".
— COTU KENYA (@COTU_K) May 28, 2021
They detest hard work and success that is merit based. The SG of @COTU_K has selflessly rendered his service to the workers of Kenya, Africa and the World thus this fete by the Nairobi County government. https://t.co/5N05OXHZq5
Atwoli pia alimkashifu vikali wakili tajika Ahmednasir Abdullahi almaarufu kama Grand Mulla kwa kusema kuwa kupatia barabara jina la Atwoli ni aibu kubwa. Grand Mulla alidai kuwa hatua hiyo ilikuwa ya kukejeli maskini kwani Atwoli hukula na kunywa na matajiri kuonyesha kiburi kwa maskini.
My record speaks for itself. Unlike you, I am a very honest man, I work hard, I never engage in corrupt dealings, I speak my mind and I am not a billionaire (like you).
— Francis Atwoli NOM (DZA), CBS, EBS, MBS. (@AtwoliDza) May 28, 2021
My influence is out of the growth of the labour movement in Kenya. Kenyans with jobs are protected.
"Matendo yangu yanajiongelea . Tofauti na wewe, mimi ni mtu mwaminifu, natia bidii na sijihusishi na mipango ya ufisadi, naongea kilicho akilini mwangu na mimi sio bilionea kama wewe. Ushawishi wangu ni kutokana na kukuza muungano wa wafanyakazi nchini. Kazi za Wakenya zimelindwa" Atwoli alimjibu Nasir.