Mama aliyeenda kulalamikia gavana Waiguru apigwa mangumi na mlinzi

Kabla ya tukio hilo kuibuka, mama huyo ambaye alionekana kuwa na ujasiri mwingi alikuwa akieleza gavana Waiguru kuhusu mashinda zinazokumba wakazi wa wadi ya Kangai

Muhtasari

•Imeripotiwa kuwa mpiga kura huyo  aliyetambulishwa kama Damaris alikuwa analalamikia ugamvi duni wa rasilimali katika Kaunti ya Kirinyaga.

•Walinzi wa gavana walikuwa walikuwa wanamzuia mwanamke huyo kufikia Gavana kwani alionekana akikaribia gari lake kwa hasira.

Mama akieleza malalamiko kwa gavana Waiguru
Mama akieleza malalamiko kwa gavana Waiguru
Image: Hisani

Hasira imeelekezwa kwa Gavana wa Kirinyaga Anne Mumbi Waiguru baada ya video inayoonyesha mmoja wa walinzi wake akipiga mwanamke.

Kwenye video hiyo, mwanamke anayesikika akitoa malalamiko kwa gavana Waiguru anaonekana kupigwa mangumi na mmoja wa mlinzi wakati anajaribu kukaribia gari la gavana.

Imeripotiwa kuwa mpiga kura huyo  aliyetambulishwa kama Damaris alikuwa analalamikia ugamvi duni wa rasilimali katika Kaunti ya Kirinyaga.

“Sio pesa nataka mimi, nimejitafutia zangu tayari. Mbona wananisukuma na hatahawapigi kura? Huyu hapa hata labda hana kura ya Kirinyaga(akionyesha mmoja wa walinzi wa gavana}” Mama huyo anasikika akilalamika kudhulumiwa na walinzi wa gavana kabla ya mmoja wao kumvamia kwa mangumi.

Follow & Subscribe Channel 7 News TV https://twitter.com/channel7newsTV https://www.facebook.com/channel7newstv https://www.instagram.com/channel7newstv http://www.youtube.com/c/CHANNEL7NEWSTV Copyright Disclaimer: Under Section 107 of the Copyright Act 1976, allowance is made for fair use for purposes such as criticism, comment, news reporting, teaching, scholarship, and research.

Walinzi wa gavana walikuwa walikuwa wanamzuia mwanamke huyo kufikia Gavana kwani alionekana akikaribia gari lake kwa hasira.

Mwanamke huyo aliendelea kusisitiza kuwa sio pesa alitaka kumuomba gavana ila alitaka kueleza malalamiko yake  huku raia waliokuwa wanashuhudia tukio hilo wakijaribu kutenganisha wawili hao.

Kabla ya tukio hilo kuibuka, mama huyo ambaye alionekana kuwa na ujasiri mwingi  alikuwa akieleza gavana Waiguru kuhusu mashinda zinazokumba wakazi wa Kangai

Tumeishio kukutafuta ila hatujawahi kuona. Mungu ni mwema nikikuwa natoka shambani nikaambiwa kuwa unafunza huku. Nilipata na vijana hawa pande za Kagio nikawaambia tuandamane hapa tueleze mashida zetu kwako kwani tutakufa pande hii ya Kangai kwa sababu ya mashida” Mama huyo alisikika akiambia gavana.

“Sisi hatujui mambo ya samaki, wewe unafunza kuhusu samaki. Hatujui mambo ya kuku, hayo ndo unafunza. Mtu wa Mungu ni kuongea. Tunakupenda sana” aliendelea kusema.

Alilalimika kuwa hakuna kituo cha afya katika wadi ya Kangai na kuwa waliteseka sana kupata matibabu.

Gavana Waiguru alikuwa ameenda kuzindua mradi wa kufuga samaki unaotazamiwa kuongeza ukulima wa samaki katika Kaunti hiyo.