logo

NOW ON AIR

Listen in Live

19% pekee ya Wakenya wangepiga kura kupitisha BBI iwapo kura ya maoni ingefanyika leo- Utafiti

Utafiti huo ambao ulikamilika Jumatatu umeonyesha kuwa BBI inaungwa mkono zaidi na wanachama wa ODM ikilinganishwa na wale wa Jubilee na UDA

image
na Radio Jambo

Patanisho01 July 2021 - 11:10

Muhtasari


•Utafiti wa hivi karibuni ambao ulifanywa na Tifa umeashiria kuwa asilimia 31% kati ya sampuli ya watu1500 ambao walitumika kufanya utafiti ungepiga kura ya 'La'

Mchanganuzi wa siasa Tom Wolf akihutubia waandishi wa habari kuhusiana na utafti wa BBI jijini Nairobi mnamo Julai 1,2021

Habari na Moses Odhiambo

Wakenya wengi wangepiga kura kupinga mchakato wa BBI iwapo kura ya maoni ingefanyika hivi leo, utafiti umebaini.

Utafiti wa hivi karibuni ambao ulifanywa na Tifa umeashiria kuwa asilimia 31% kati ya sampuli ya watu1500 ambao walitumika kufanya utafiti ungepiga kura ya 'La'

Asilimia kidogo ya 19% wangepiga kura kupitisha mchakato huo, asilimia 18% walisema kuwa hawangepiga kura ilhali 14% hawajafanya maamuzi.

Utafiti huo ambao ulikamilika Jumatatu umeonyesha  kuwa BBI inaungwa mkono zaidi na wanachama wa ODM ikilinganishwa na wale wa Jubilee na UDA.

Utafiti huo ulifanywa kwa njia ya mahojiano ya  simu kwa watu ambao nambari zao zilichukuliwa kwa njia ya moja kwa moja.

Kiwango cha kosa cha utafiti huo ni +/-2.53%.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved