logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Ni wazimu kuwa jamaa ataka kuniua pamoja na walio karibu nami juu amekataliwa!' Lilian Ng'anga asikitishwa na vitisho vya Mutua

Kulingana na mpenzi huyo wa Juliani, kitendo cha gavana  Mutua cha kutishia kumuua pamoja na walio karibu naye kwa sababu alimkataa ni kitendo cha kale.

image
na Radio Jambo

Habari07 November 2021 - 08:48

Muhtasari


•Kupitia ujumbe ambao alichapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram asubuhi ya Jumapili, Lilian amesema angependa kuwe na amani kati yake na gavana Mutua ila sio kisasi.

•Kulingana na mpenzi huyo wa Juliani, kitendo cha gavana  Mutua cha kutishia kumuua pamoja na walio karibu naye kwa sababu alimkataa ni kitendo cha kale.

•Lilian ameeleza uhusiano wake na mgombeji huyo wa kiti cha urais mwaka ujao ulivyokuwa huku akisisitiza hawakuwa mume na mke.

Lilian Ng'anga ameendelea kuzungumza kuhusu masaibu yayiyofuata baada ya utengano wake na gavana wa Machakos  Alfred Mutua mapema mwaka huu.

Huku wawili hao wakionekana kuwa na uhusiano mbaya katika kipindi cha miezi michache iliyopita, Lilian amedai kuwa mapenzi yake ni watengane vizuri kama watu wazima.

Kupitia ujumbe ambao alichapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram asubuhi ya Jumapili, Lilian amesema angependa kuwe na amani kati yake na gavana Mutua ila sio kisasi.

"Mimi ningependa tuwe na utengano mzima na wenye urafiki. Ningependa amani kati yetu na mwishowe tuwe marafiki, baada ya yote tumekuwa pamoja kwa mwongo mmoja" Lilian amesema.

Kulingana na mpenzi huyo wa Juliani, kitendo cha gavana  Mutua cha kutishia kumuua pamoja na walio karibu naye kwa sababu alimkataa ni kitendo cha kale.

"Ni wazimu kuona mwanaume anataka kuniua na watu walio karibu nami kwa sababu nilisema HAPANA. Kitenda cha kale vipi!" Amesema Lilian.

Pia amefutulia mbali madai kuwa alisababisha kuvunjika kwa ndoa ya kwanza ya Mutua mwongo mmoja uliopita huku akieleza kwamba tayari ilikuwa imevunjika kitambo kabla hajajitosa kwenye mahusiano na gavana huyo.

Lilian ameeleza uhusiano wake na mgombeji huyo wa kiti cha urais mwaka ujao ulivyokuwa huku akisisitiza hawakuwa mume na mke.

"Alichokuwa amefanya Alfred ni "Kuhanda ithege" ikija kwa ndoa. Najua, naheshimu na kukubali kuwa kushirikiana kwaweza kuitwa ndoa lakini hatukuwahi tia saini kwenye karatasi zozote kuonyesha kuwa tulikuwa tumefunga ndoa kihalali.  Hatukufunya jambo lolote la kitamaduni ambalo lingetufanya mume na mke" Lilian ameeleza.

Amesema kuwa inasikitisha kuona wanawake wakidhalilishwa katika jamii huku akishinikiza watu kubali tamaduni hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved