logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzia: Radi yaua mtoto Bungoma

Visa vya vifo vya radi vimeongezeka eneo hilo jambo ambalo limelazimu shule kuweka vifaa vya kudhibiti radi.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri26 November 2021 - 07:25

Muhtasari


• Mwanafunzi wa darasa la Saba katika shule ya msingi ya Buema, katika kata ya Musikoma, eneo bunge la Kanduyi alifariki dunia baada ya kupigwa na radi siku ya Alhamisi. 

• Alikuwa amerejea kutoka shuleni na alikuwa akiwalisha sungura wake kisa hicho kilopotokea.

• Babake marehemu alisema mwanafunzi huyo alichuna mboga na kuanza kuwalisha sungura wake lakini kukatokea radi kali. 

Mwanafunzi wa shule ya msingi alifariki papo hapo katika Kaunti ya Bungoma baada ya kupigwa na radi. 

Mwanafunzi wa darasa la Saba katika shule ya msingi ya Buema, katika kata ya Musikoma, eneo bunge la Kanduyi alifariki dunia baada ya kupigwa na radi siku ya Alhamisi. 

Alikuwa amerejea kutoka shuleni na alikuwa akiwalisha sungura wake kisa hicho kilopotokea.  Babake marehemu alisema mwanafunzi huyo alichuna mboga na kuanza kuwalisha sungura wake lakini kukatokea radi kali. 

“Dada yake alitoka kwenda kumuita ili tupate chakula cha jioni pamoja lakini alimkuta amelala, jitihada za kumwamsha hazikufua dafu kwani hakuitikia,” alisema.

 Alikimbizwa hospitali lakini alikuwa tayari amefariki. 

"Nimesikitishwa na kifo chake, alikuwa kijana mchapakazi ambaye nilikuwa na matumaini mengi sana kwake, sielewi nani ataziba pengo," alisema babake huku akitiririkwa. 

Visa vya vifo vya radi vimeongezeka eneo hilo jambo ambalo limelazimu shule kuweka vifaa vya kudhibiti radi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved