logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Moses Kuria abadili msimamo, aapa kupigia debe BBI

Kuria amesema tatizo kubwa la BBI lilikuwa mchakato wake ila sio maudhui yake.

image
na Radio Jambo

Habari31 March 2022 - 05:15

Muhtasari


•Mwandani huyo wa naibu rais William Ruto amesema tatizo kubwa la BBI lilikuwa mchakato wake ila sio maudhui yake.

Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria

Mbunge wa Gatundu Kusini, Moses Kuria, ameapa kuwa katika mstari wa mbele kupigia debe BBI ikiwa mahakama ya upeo itaidhinisha mchakato wake.

Mwandani huyo wa naibu rais William Ruto amesema tatizo kubwa la BBI lilikuwa mchakato wake ila sio maudhui yake.

"Tatizo la BBI halikuwa maudhui pekee; lilikuwa ni mchakato. Athari halisi ya uamuzi wa mahakama ya upeo leo ​​itakuwa suluhu kwa matatizo yote ya mchakato. Ikiwa mahakama ya upeo itaamuru kupendelea BBI, hiyo itasafisha mchakato huo," Kuria alisema kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Kuria ambaye ni mmoja wa wanasiasa waliopinga vikali BBI mwaka jana amesema yupo tayari kusukuma utekelezaji wake mara moja mahakama ikiipitisha.

Mahakama ya juu zaidi inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu BBI hivi leo, takriban miezi saba baada ya mahakamu kuu kutupilia mbali mchakato huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved