logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanga apewa tikiti ya moja kwa moja na ODM kuwania ugavana Homabay

Wanga apewa tikiti ya moja kwa moja na ODM kuwania ugavana Homabay.

image
na Radio Jambo

Mahakama31 March 2022 - 13:13

Muhtasari


• Gladys Wanga ateuliwa kama mgombeaji wa ugavana kaunti ya Homabay kupitia tikiti ya ODM.

• Raila Odinga alisema uamuzi huo uliafikiwa baada ya mazungumzo ya kina na viongozi wa chama hicho.

Mwakilishi wa kina mama katika kaunti ya Homabay, Gladys Wanga amepewa tikiti ya moja kwa moja na chama cha ODM kuwania wadhfa wa ugavana katika kaunti hiyo.

Kupitia ujumbe uliotolewa na  kinara wa chama Raila Odinga, kulikuwa na wawaniaji wengine saba  ambao walilazimika kujiondoa katika kinyang'anyiro hicho na kumuunga mkono Wanga.

Aidha, mheshimiwa Oyugi Magwanga aliteuliwa kama mgombea mwenza wa Gladys Wanga.

Odinga alisema kwamba katiba ya chama hicho inawarusu kumchagua mgombea wao baada ya kufanya mazungumzo ya kina.

Viongozi wote sasa walitakiwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha wanaibuka kidedea katika uchaguzi wa Agosti 9.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved