logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jina la kampuni ya Kijapani lilivyozua taharuki mitandaoni

Jina la kampuni hiyo ya vyombo vya habari lina maana ''hana sehemu za siri'' kwa kiswahili.

image
na Radio Jambo

Habari23 June 2022 - 04:40

Muhtasari


• Neno hilo kwa kawaida si la staha kutamkwa hadharani kwa maana ya Kiswahili.

Wakenya wengi mtandaoni na wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili kwingineko wanaelezea mshtuko wao na wakizua mjadala kuhusu jina la kampuni mpya ya Naomi Osaka iliyozinduliwa.

Jina la kampuni ya vyombo vya habari lenye maana ''hana sehemu za siri'' kwa kiswahili ambayo Osaka amezindua kwa ushirikiano na bingwa mara nne wa NBA LeBron James - imezua taharuki na imekuwa ikivuma kwenye mtandao waTwitter.

Neno hilo kwa kawaida si la staha kutamkwa hadharani kwa maana ya Kiswahili.

Vyombo kadha vya habari nchini Kenya, vimeandika kuhusu mada hiyo vikihoji kwa nini Wakenya wamekuwa wakijadili kwa kiasi kikubwa mtandaoni jina la kampuni hiyo.

Kampuni ya utayarishaji imesema itakuwa ikitengeneza hadithi ambazo "ni maalum kitamaduni lakini za ulimwengu kwa watazamaji wote" na zinalenga "kushughulikia masuala muhimu ya jamii".


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved