logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shule ya upili yamulikwa kwa madai ya kuwanyima wanafunzi chakula

Wazazi na jamii waliripoti kuwa wanafunzi waliokuwa na madeni ya walikuwa wakinyimwa chakula.

image
na

Makala31 July 2022 - 07:38

Muhtasari


•Wazazi wa shule ya upili ya Ambira wamemshtumu Mkuu wa Shule Joseph Otieno kwa kuwanyima chakula wanafunzi walio na deni.

•Mkuu wa shule, hata hivyo, alikanusha madai hayo akisema kuwa kila kitu kilikuwa kikienda sawa huko Ambira.

Baadhi ya wazazi wa shule ya upili ya Ambira wamemshtumu Mkuu wa Shule Joseph Otieno kwa kuwanyima chakula wanafunzi walio na deni la karo ya shule.

Otieno hata hivyo amekana madai hayo.

Wazazi na jamii waliripoti kuwa wanafunzi waliokuwa na malimbikizo ya karo ya shule kwa muhula wa pili walikuwa wakinyimwa chakula.

Ilidaiwa kuwa wanafunzi hao hawakuruhusiwa kuingia madarasani na hawakutumwa nyumbani pia.

Mzazi Jane, sio jina lake halisi, alisema kwamba alitembelea shule hiyo siku ya Ijumaa baada ya kupokea habari za kuhuzunisha kwamba mtoto wake alikuwa na njaa.

"Watoto wetu walikuwa wakipiga simu nyumbani kuripoti kwamba hawakuwa wakihudhuria masomo, wakinyimwa chakula na hawaruhusiwi kwenda nyumbani," alisema.

Aliripoti kuwa Otieno alitishia kutekeleza azma yake kwenye kikundi cha WhatsApp cha shule hiyo lakini wazazi wakapuuzilia suala hilo.

“Niliwapata wanafunzi wakiwa wachafu, wamelala uwanjani na hawakuwa wamekula,” alisema Jane ambaye alikuwa amesafiri kutoka Kaunti ya Busia.

Alisema kuwa kantini ya shule hiyo ilianza kufanya kazi kuanzia saakumi na mbili jioni na paliuzwa mikate na soda pekee.

Jane, alisema kwa upande wake, alilipa malimbikizo ya ada kupitia nambari ya malipo ya taasisi hiyo lakini mtoto wake bado alikuwa amewekwa njaa kama wengine.

Mzazi mwingine, ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema kwamba alipokea simu ya kuhuzunisha kutoka kwa mwanawe Ijumaa jioni.

Mwanawe alimweleza kuwa yeye na wenzake walikuwa wamejikinga chini ya mti licha ya mvua kubwa iliyonyesha baada ya kutolewa nje ya masomo na kunyimwa fursa ya kurejea nyumbani.

Mkuu wa shule, hata hivyo, alikanusha madai hayo akisema kuwa kila kitu kilikuwa kikienda sawa huko Ambira.

"Wanafunzi walipata kifungua kinywa, chakula cha mchana na chakula cha jioni. Hakuna mtu…

Alibainisha kuwa wanafunzi hao wamekuwa wakishiriki na kushinda michezo ya mpira; jambo ambalo si la kawaida na wachezaji ambao hawajala.

“Jana walipiga shule moja 5:0, nyingine 4:0 na leo tunaenda fainali. Niliwaambia wazazi waliokuja shuleni kulipa ada lakini watoto wao wako shuleni.

Waziri wa Elimu George Magoha ameendelea kuwaagiza wakuu wa shule kutomfukuza mwanafunzi yeyote kwa kutolipa karo.

Akizungumza katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Mbaga mnamo Julai 16, Magoha alisema kuwa shule zote nchini zitakuwa na fedha za kufundishia katika akaunti zao kufikia Jumatatu, Julai 18, hivi punde.

Kwa fedha hizo, Waziri Mkuu alibainisha kuwa wakuu wanapaswa kuwa na uwezo wa kuendesha shule bila kusimamisha masomo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved