logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gari la gavana Mutula lahusika kwenye ajali mnamo siku ya kuapishwa

Gari hilo lilipoteza udhibiti kabla ya kutua kwenye mtaro.

image
na Radio Jambo

Habari25 August 2022 - 11:02

Muhtasari


•Ajali hiyo ilitokea katika Barabara ya Machakos-Wote karibu na Wote Town mwendo wa saa nne unusu asubuhi.

•Kilonzo alitumia gari tofauti kufika eneo la tukio la kuapishwa.

Gari la gavana mteule wa Makueni Mutula Kilonzo Junior lilihusika katika ajali likielekea kwenye hafla ya kuapishwa.

Gari la gavana wa Makueni Mutula Kilonzo Junior lilihusika katika ajali kabla ya hafla ya kuapishwa kwake.

Ajali hiyo ilitokea katika Barabara ya Machakos-Wote karibu na Wote Town mwendo wa saa nne unusu asubuhi.

Duru za kuaminika ziliarifu kuwa watu watatu waliokuwa ndani waliweza kunusurika bila majeraha.

Mutula hakuwa miongoni mwa watu waliokuwa kwenye gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser V8 wakati ajali ilipotokea.

Gari la gavana mteule wa Makueni Mutula Kilonzo Junior lilihusika katika ajali likielekea kwenye hafla ya kuapishwa.

Kilonzo alitumia gari tofauti kufika eneo la tukio la kuapishwa.

Inasemekana gari hilo lilipoteza udhibiti kabla ya kutua kwenye mtaro.

Mengine yanafuata...


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved