logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fuliza! Ada ya mikopo ya fuliza yapunguzwa kwa 50%

Safaricom Ilitangaza kupunguzwa kwa ada za mkopo wa Fuliza kwa asilimia 50.

image
na

Yanayojiri28 September 2022 - 13:38

Muhtasari


• Hatua hii inatarajiwa kunufaisha angalau asilimia 80 ya wakopaji milioni 28 kwenye jukwaa ambalo lilizinduliwa na Safaricom na benki hizo mbili mwaka 2019.

Mashirika ya Safaricom, KCB na NCBA yamefutilia mbali ada za utunzi wa mfumo zilizokuwa zikitozwa wateja wa Fuliza wanaokopa chini ya Shilingi 1,000 kwa siku tatu za kwanza.

Hatua hii inatarajiwa kunufaisha angalau asilimia 80 ya wakopaji milioni 28 kwenye jukwaa ambalo lilizinduliwa na Safaricom na benki hizo mbili mwaka 2019.

Akizungumza wakati wa mkutano uliohudhuriwa na Rais William Ruto, Afisa mkuu mtendaji wa Safaricom Peter Ndegwa alitangaza kupunguzwa kwa ada za mkopo wa Fuliza kwa asilimia 50.

"Hii inatarajiwa kupunguza gharama za mikopo na ufikiaji kwa nusu kwa wateja wetu tunapotembea katika safari ya ujumuishaji wa kifedha," Ndegwa alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved