logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jumba la ghorofa 8 la poromoka Tasia,Embakasi

Hakuna majeruhi walioripotiwa kufikia sasa.

image
na Radio Jambo

Makala07 November 2022 - 16:49

Muhtasari


  • Mnamo Septemba, watu wawili waliaga dunia na saba kuokolewa baada ya nyumba ya ghorofa sita iliyokuwa ikijengwa kuporomoka katika eneo la Kirigiti, Kaunti ya Kiambu

Jengo la ghorofa nane limeporomoka Kwa-Ndege, Tassia, Embakasi.

Kikosi cha uokoaji kutoka Msalaba Mwekundu kwa sasa kiko kwenye eneo la tukio kwa uokoaji.

Kulingana na nduru za habari ghorofa ya chini na ghorofa ya kwanza ya jengo hilo iliathirika pakubwa.

"Jengo lilipoanza kuporomoka, watu walihama," shahidi aliambia vyombo vya habari.

Hakuna majeruhi walioripotiwa kufikia sasa.

Jengo hilo lilikuwa na biashara katika ghorofa ya chini.

Mnamo Septemba, watu wawili waliaga dunia na saba kuokolewa baada ya nyumba ya ghorofa sita iliyokuwa ikijengwa kuporomoka katika eneo la Kirigiti, Kaunti ya Kiambu.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved